Mwenyekiti wa Bodi ya
Usajili wa Wahandisi nchini (ERB), Mhandisi, Profesa Ninatubu Lema, akisisitiza
jambo wakati wa kufunga Mkutano wa 15 wa mwaka wa wahandisi uliofanyika leo
mjini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara
ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhandisi Joseph
Nyamhanga, akizungumza na wahandisi
(hawapo pichani), wakati wa kufunga Mkutano wa 15 wa mwaka wa wahandisi
uliofanyika leo mjini Dodoma.
Baadhi ya wahandisi
wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta
ya Ujenzi), Mhandisi Joseph Nyamhanga (hayupo pichani), wakati wa kufunga
Mkutano wa 15 wa mwaka wa wahandisi uliofanyika leo mjini Dodoma.
Kaimu Msajili
wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi
nchini (ERB), Mhandisi Patrick Barozi,
akisoma maazimio yaliyofikiwa katika Mkutano wa 15 wa mwaka wa wahandisi
uliofanyika mjini Dodoma
Katibu Mkuu wa wa
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhandisi Joseph
Nyamhanga, akimkabidhi cheti mmoja wa watoa huduma aliyefanya vizuri katika
utoaji wahuduma bora kwenye Mkutano wa 15 wa mwaka wa wahandisi uliofanyika leo
mjini Dodoma. Wa tatu kulia ni Mkurugenzi wa Barabara kutoka Sekta hiyo Mhandisi
Ven Ndyamukama, akishuhudia tukio hilo.
...
Katibu Mkuu wa Wizara
ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhandisi Joseph Nyamhanga,
amezungumzia umuhimu wa Wizara, Taasisi na Idara za Serikali kutumia vifungu
vilivyopo kwenye sheria ya ununuzi wa umma ya mwaka 2011 na kanuni za ununuzi
wa umma za mwaka 2013 na marekebisho yake ya mwaka 2016.
Sheria hiyo inawapa
fursa makandarasi wazalendo, watalamu washauri, wa zabuni na watoa huduma
mbalimbali kupata fursa nyingi katika miradi mbalimbali ya ujenzi hapa nchini.
Akifunga maadhimisho
ya 15 ya Wahandisi mjini Dodoma, Mhandisi Nyamhanga, amesema chini ya sheria ya
sasa miradi isiyozidi bilioni 10 imewekewa utaratibu mzuri wa kutekelezwa na
makandarasi wazalendo na hivyo kuwawezesha kukuza uwezo wa kitaaluma na
kiuchumi.
"Hakikisheni
mnapopata miradi hii mnafanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia muda na thamani ya
fedha ili kuongeza tija katika miradi yenyewe na kutoa fursa kwa miradi mikubwa
kupewa makandarasi wazalendo", amesema Mhandisi Nyamhanga.
Amewataka wahandisi
kutumia maadhimisho ya 15 kama somo la kukabiliana na changamoto mbalimbali
zinazolikabili Taifa ili kufikia malengo ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati yenye viwanda na
rasilimali watu wenye weledi wa kisasa.
Aidha, ametoa wito kwa Bodi ya Usajili ya Wahandisi (ERB), kutoa kipaumbele kwa
wanafunzi waliohitimu katika kozi ya kihandisi kwa kugharamia mafunzo kwa
vitendo kwa kutumia fedha zinazotolewa na Serikali na zile za wafadhili ili
kuweza kuendeleza taaluma kwa Wahandisi.
"Wizara
itaendelea na mkakati wake wa kufadhili mafunzo kwa vitendo na kuhakikisha
wahitimu wa vyuo mbalimbali vya wahandisi nchini wanakidhi mahitaji soko la
ajira ndani na nje ya nchi", amesisitiza Mhandisi Nyamhanga.
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa Bodi ya ERB, Mhandisi Profesa Ninatubu Lema, amewapongeza watoa
mada wote walioshiriki katika maadhimisho ya 15 na kuahidi bodi hiyo
itayafanyia kazi mafunzo hayo na kuhakikisha kila mhandisi ananufaika na
mafunzo hayo.
katika maadhimisho
hayo wahandisi wamepata fursa ya kujifunza maswala ya utafiti na maendeleo,
ubunifu, masoko na ujasiriamali, maendeleo ya viwanda na utunzaji wa mazingira,
na uharakishaji wa Teknolojia, habari na mawasiliano kijamii, kiuchumi na
kimaendeleo.
Naye Kaimu Msajili wa
Bodi ya ERB, Mhandisi Patrick Barozi, amesema bodi hiyo imejipanga kikamilifu
kuhakikisha wahandisi wanapata mazingira mazuri ya kufanya kazi ndani na nje ya
nchi kwa kuzingatia weledi, uadilifu na ubora unaopimika.
Maadhimisho ya 15 ya
Wahandisi yaliyofunguliwa jana na Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Balozi John
Kijazi na kufungwa leo na Katibu Mkuu (Sekta ya Ujenzi), Mhandisi Joseph
Nyamhanga yamelenga kuwakutanisha wahandisi kujadili kwa pamoja "Jukumu la
Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati katika Kukuza Viwanda kwa Maendeleo
ya Kijamii na Kiuchumi",
Imetolewa na Kitengo
cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano





0 Comments