Random Posts

Waziri Ummy alaani jaribio la kuwauwa Wanawake wanne kwa kuwachoma moto Mkoani Tabora

Waziri ametoa rai kwa jamii kuacha mila zinazomgandamiza mwanamke ili kuondokana na vitendo vya ukatili wa kijinsia vinavyotokana na imani za kishirikina. Ameiasa jamii kufanya kazi kwa bidii na weledi ili kuboresha maisha yao na kutokomeza imani potofu  zinazoendeleza ukatili na mauaji ya wanawake jambo linalodhohofisha juhudi za Serikali katika kuhakikisha kuwa jamii zetu zinakuwa na mazingira salama ya kuishi kwa kila Mtanzania akiwemo Mwanamke.

Mhe. Ummy Mwalimu ameitaka jamii itambue kuwa hakuna mwenye haki ya kukatisha uhai wa mtu mwingine kitendo cha kukatisha uhai wa mtu kwa shambulio kama hili ni kosa kisheria na Serikali itahakikisha wote wanaohusika na vitendo kama hivi, hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao. Kadhalika, Waziri Ummy amepongeza Jeshi la Polisi Mkoani Tabora kwa kufika sehemu ya tukio na kuwaokoa wanawake hao muda mfupi kabla ya jaribio la kuteketezwa kwa moto kufuatia kuwepo kwa tuhuma za kishirikina.

Mhe. Waziri anatoa pole kwa wanawake hao pamoja na familia zao. Aidha anawaomba kuwa na moyo wa subira na uvumilivu wakati mamlaka zinalichunguza shauri hili.  

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

22/09/2017

Post a Comment

0 Comments