Mkurugenzi
wa Idara ya Habari(MAELEZO ) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abassi akisikiliza
jambo kutoka kwa Mama Maria Nyerere kuelekea kumbukizi ya miaka 18 ya Baba wa
Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wakati wa mahojiano maalum na Mjane huyo
nyumbani kwake Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari(MAELEZO )
na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abassi akifanya mahojiano na Mama Maria
Nyerere kuelekea kumbikizi ya Baba wa Taifa , Mjane huyo aliwasisitiza vijana
kuzingatia michezo na utamaduni.
(picha na Paschal Dotto- MAELEZO
.....
Na.Paschal
Dotto-MAELEZO
Mama Maria Nyerere amewaasa
vijana kuzingatia utamaduni na michezo ili kuweka sawa akili yao na kuendelea
na ujenzi wa taifa kwani michezo hukutanisha watu wengi na kuwawezesha
kubadilishana mawazo yenye kujenga katika maisha.
Akizungumza leo na
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Dkt. Hassan Abbasi nyumbani kwake
Jijini Dar es Salaam, Mama Maria Nyerere alisema kuwa michezo ni hatua muhimu
ya ukombozi wa fikra kwa vijana kwani wakizingatia michezo wataweza kufanya
kazi na kujipatia mahitaji muhumi kama chakula na kuondokana na dhana ya utegemezi.
“Vijana wamajikita
katika mambo maovu, sasa kitakachoweza kusaidia ni michezo kwani
inawachangamsha, kuwakutanisha na kuweza kubadilishana mawazo mazuri na kwa
sasa wanaendelea vyema na masuala haya ya michezo ambayo yanadumisha pia
utamaduni,” alisema Mama Maria
Aidha, Mjane wa Hayati
Baba wa Taifa alisema kuwa kwa sasa vijana wameanza kujirudi katika kudumisha
utamaduni kwani walitaka kupotoka na kuacha utamaduni wao, alieleza kuwa watoto
wanazaliwa bila ukomavu wa akili katika utamaduni, lakini pia hawapati elimu ya
kutosha kutoka kwa wazazi kuhusu utamaduni matokeo yake ni kuishia kuwa na watu
wenye tabia za ajabu.
“Kitakachoweza
kuwasaidia vijana wetu ni kuwafundisha utamaduni wetu ili wawe na maadili kwani
sasa hivi mtoto anazaliwa hapati elimu ya utamaduni wake, wazazi wametupa
utamaduni mbali, ni lazima mtoto atakuwa na tabia za ajabu ajabu,”alisisitiza Mama
Maria Nyerere.
Aliongeza kuwa jukumu la ukombozi wa vijana kutoka
katika vitendo vibovu ni la watanzania wote kuweza kuwaelimisha vijana kuhusu
michezo ili kuweka akili zao sawa katika kuzalisha na kusaidia kujipatia kipato chao na taifa kwa ujumla.
Mama Maria Nyerere
alisema kuwa kujitegemea kwa vijana hasa katika kufanya kazi kutawawezesha
kutimiza ndoto zao na za taifa lenye uchumi wa viwanda kwa ujumla.


0 Comments