Waziri
wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akifungua mkutano
wa 28 wa wadau wa bodi ya usajili wa wabunifu majengo na wakadiriaji wa majenzi wa siku mbili katika ukumbi wa mlimani city jijini Dar es Salaam Oktoba 12-13 2017, lengo la mkutano huo ni kujifunza
mambo mapya yanayotokea katika utendaji sekta ya ujenzi.
Waandishi wa habari wakiwa kazini.
Wadau wa bodi ya usajili wa wabunifu majengo na wakadiriaji wa majenzi wakiwa katika mkutano wa siku mbili katika ukumbi wa mlimani city jijini Dar es Salaam Oktoba 12-13 2017, lengo la mkutano huo ni kujifunza mambo mapya yanayotokea katika utendaji sekta ya ujenzi.
Kaimu Msajili wa bodi ya usajili wa wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi Albert Munuo akielezea mpango wa mafunzo endelevu wakati wa mkutano wa siku mbili katika ukumbi wa mlimani city jijini Dar es Salaam Oktoba 12-13 2017, lengo la mkutano huo ni kujifunza mambo mapya yanayotokea katika utendaji sekta ya ujenzi.
Mashaka Mbundala akifafanua jambo
Afisa Mkuu Ukaguzi wa Ndani wa bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji wa Majenzi, Ezekiel Stephen (katikati) akiwa pamoja na wadau wengine wakifuatilia mada mbalimbali katika mkutano huo.
Wadau wakiwa kwenye mkutano.

Afisa Masoko wa Kampuni ya Knauf Gypsum Tanzania, Bi Irene Mwakapugi (kushoto) akielezea utengenezaji dari kwa kutumia chuma badala ya mbao (kulia) Meneja Masoko wa Kampuni hiyo, Rachel Zhong.
Wadau mbalimbali wakijiandikisha kabla ya kuingia ukumbini.
Watumishi wa bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji wa Majenzi.
Afisa Masoko wa Kampuni ya Knauf Gypsum Tanzania, Bi Irene Mwakapugi (kushoto) akielezea utengenezaji dari kwa kutumia chuma badala ya mbao (kulia) Meneja Masoko wa Kampuni hiyo, Rachel Zhong.
Wadau mbalimbali wakijiandikisha kabla ya kuingia ukumbini.
Watumishi wa bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji wa Majenzi.
Kaimu Msajili wa bodi ya usajili wa wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi Albert Munuo (aliyeweka mkono mfukoni) akisikiliza jambo kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo DKT.Ambwene Mwakyusa.
Muonekano wa mabanda katika mkutano wa siku mbili katika ukumbi wa mlimani city jijini Dar es Salaam Oktoba 12-13 2017,
Waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (kushoto) akipewa maelezo kutoka mmoja wa wadau wabunifu majengo na wakadiriaji wa majenzi alipotembelea mabada mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa mlimani city jijini Dar es Salaam Oktoba 12-13 2017,
Waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wa bodi ya usajili wa wabunifu majengo na wakadiriaji wa majenzi wa siku mbili katika ukumbi wa mlimani city jijini Dar es Salaam Oktoba 12-13 2017, lengo la mkutano huo ni kujifunza mambo mapya yanayotokea katika utendaji sekta ya ujenzi.
..
Na Mwandishi wetu
Na Mwandishi wetu
Waziri wa ujenzi, uchukuzi
na mawasiliano Prof. Makame Mbarawa ameiagiza bodi ya usajili wa wabunifu
majengo na wakadiriaji wa majenzi kuwafutia usajili na kuwachukulia hatua kali
wataalam wote watakaobainika kupokea au kutoa rushwa katika kutekeleza wajibu
wao.
Akizungumza jijini Dar es
salaam katika ufunguzi wa mkutano wa 28 wa wadau wa bodi ya usajili wa wabunifu
majengo na wakadiriaji wa majenzi amesema kuwa ni muhimu kwa bodi kufanya
ukaguzi wa mara kwa mara katika miradi ili kubaini wale wote wanaukiuka
taratibu kwaajili ya rushwa.
Waziri MBARAWA ameipongeza
bodi hiyo kukutanisha wataalam hao na wadau wa bodi ya nchini Kenya na
kuwaasa kuendelea kukutana kubadilishana ujuzi kwakuwa teknolojia inakua kwa
kasi sana hivyo ni vema kujifunza zaidi ili kukabiliana na majanga ya
matetemeko ya ardhi.
Pia ameipongeza bodi hiyo
kwa kubuni michoro ya majengo kwa gharama nafuu na kusema kuwa
itawanufaisha watanzania katika kutatua matatizo ya ujenzi.
Aidha Profesa MBARAWA
ametoa agizo kwa wakurugenzi na watendaji wa makampuni ya sekta ya ujenzi kuhakikisha vijana wanapewa fursa ya kuwekwa katika kila sehemu yenye miradi
mkubwa ili waweze kujifunza na kunufaika kupitia miradi hiyo.
Kwa upande wake Kaimu Msajili wa bodi ya usajili wa wabunifu majengo na wakadiriaji majenzi ALBERT MUNUO
amesema kuwa semina hiyo ni mwendelezo wa mpango wa mafunzo endelevu ambazo
bodi imekuwa ikiandaa kwa lengo la kuwakutanisha wabunifu wa
majengo,wakadiriaji majenzi na wataalam wanaohusiana na sekta ya ujenzi lengo
likiwa kujifunza mambo mapya yanayotokea katika utendaji kazi.
Mkutano huo wa bodi
umewakutanisha wadau na wataalamu wa majenzi na makandarasi mada kuu ni
mbinu ya kupunguza madhara ya matetemeko ya ardhi,ukaguzi wa miradi ya ujenzi
na matengenezo ya majengo na miundombinu.
0 Comments