Akizungumza
kwenye ziara yake mjini Geita ya kuzindua kampeni ya ujenzi wa vyumba vya
madarasa na zahanati Mhandisi Luhumbi amepokea malalamiko ya wakazi wa
Machinjioni waliodai kutosomewa taarifa za mapato na matumizi ya fedha zao.
Mhandisi
Luhumbi alisema kuwa endapo kama itakabainika
kuwa kiongozi wa mtaa, kijiji au Kata ametumia vibaya fedha za wananchi
anapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria na kuzirejesha fedha hizo.
“Mkurugenzi leta timu ya ukaguzi wa hesabu za
Serikali ili ikague na kujiridhisha kama kuna fedha yoyote iliyochukuliwa
pasipo maelezo yanayojitosheleza hatua zichukuliwe haraka kwa wote
watakaobainika kuhusika". Alisisitiza
Luhumbi.
Mheshimiwa
Robert ameongeza kuwa ukaguzi huo ufanyike kuanzia mwaka 2014 hadi 2017 kisha
apate taarifa hiyo ofisini. Akiwa katika
Halmashauri hiyo Mkuu wa Mkoa amepongeza jitihada zinazofanywa na wananchi za
kushiriki katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo licha ya kuwepo
changamoto nyingi katika maeneo yao.
Diwani wa
Kata ya Mgusu Bw P
...
0 Comments