Waziri Wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.
Ummy Mwalimu akizindua Benki ya damu iliyodhaminiwa na Ubalozi wa Kuwait
leo jijini Dar es salaam akiwa na Balozi wa Kuwait Bw. Jasem Ibrahim
Al-Najem
Waziri Wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.
Ummy Mwalimu akizindua Benki ya damu iliyodhaminiwa na Ubalozi wa Kuwait
leo jijini Dar es salaam akiwa na Balozi wa Kuwait Bw. Jasem Ibrahim
Al-Najem
Balozi wa Kuwait Bw. Jasem Ibrahim Al-Najem kulia akimkabidhi
zawadi ya mchango mkubwa katika Wizara ya Afya Mhe. Ummy Mwalimu kushoto
wakati wa uzinduzi wa Benki ya damu iliyodhaminiwa na Ubalozi wa Kuwait
leo jijini Dar es salaam.
Waziri Wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.
Ummy Mwalimu aliyesimama akiongea na baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya
Mifupa nchini MOI wakati wa uzinduzi wa Benki ya damu iliyodhaminiwa na
Ubalozi wa Kuwait leo jijini Dar es salaam, Kulia ni Balozi wa Kuwait
Bw. Jasem Ibrahim Al-Najem.
Balozi wa Kuwait Bw. Jasem Ibrahim Al-Najem aliyesimama akiongea
na baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Mifupa nchini MOI wakati wa
uzinduzi wa Benki ya damu iliyodhaminiwa na Ubalozi wa Kuwait leo jijini
Dar es salaam , katikati waliokaa ni Waziri Wa Afya,Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu na anayefuata ni Mkurugenzi
wa Taasisi hiyo Dkt. Respicious Lwezimula.
Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Mifupa nchini MOI
wakimsikiliza kwa makini ni Waziri Wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu hayupo pichani wakati wa uzinduzi wa
Benki ya damu iliyodhaminiwa na Ubalozi wa Kuwait leo jijini Dar es
salaam.
Mwanachama wa Kikundi cha Kutayarisha Madereva wa Magari
Makubwa Wanawake (WOW) Afrika Mashariki Bi. Rehema Mwangolombe akiwa
katika maandalizi ya kuchangia damu damu katika Benki ya damu mpya
iliyozinduliwa na Waziri Wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi huo uliyofanyika leo jijini
Dar es salaam.
Balozi wa Kuwait Bw. Jasem Ibrahim Al-Najem akichangia damu katika uzinduzi wa benki ya damu leo.
PICHA NA ALLY DAUD- WAMJW
......
NA WAMJW-DAR ES SALAAM.
WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya
Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu ameendelea kusisitiza
kuwa wananchi hawapaswi kununua damu kwani huduma hiyo ni bure kwa
watanzania wote katika hospitali zote.
Hayo amezungumza leo jijini Dar
es salaam wakati wa uzinduzi wa Benki ya damu iliyodhaminiwa na
Ubalozi wa Kuwait katika Taasisi ya Mifupa MOI ambapo uliuzuliwa na
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania.
“Watanzania wanahoitaji huduma ya
kuongezewa damu wapewe bure marufuku kwa watoa huduma za vituo vya afya
pamoja na hospitali zote kuuza damu hiyo kwani inatoka kwa wananchi
wenyewe” alisisitiza Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa
wananchi wanatakiwa kujitokeza katika kuchangia damu ili kuweza kuwa na
hifadhi ya kutosha na kufanya kazi kwa wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo
kwa wakati sahihi bila ya usumbufu wowote katika kuokoa maisha ya
watanzania.
Mbali na hayo Waziri Ummy
amesema kuwa anayo furaha kutimiza miaka miwili tangu kuingia kwa
Serikali ya awamu ya tano kwa kupiga hatua katika sekta ya afya hasa
katika kupunguza rufaa za nje na kuwa na utaalamu wa matibabu ya
kibingwa kama vile upandikizaji wa figo, vifaa vya usikivu( Coclea
Impant) na kutibu magonjwa ya moyo.
Kwa upande wake Balozi wa Kuwait
Nchini Tanzania Bw. Jasem Ibrahim Al-Najem amesema kuwa wameamua
kuchangia kiasi cha fedha cha shilingi Milioni 200 katika kutengeneza
Benki hiyo ya damu MOI ili kuweza kusaidia kuboresha sekta ya afya
nchini.
“Mbali na kiasi hicho cha fedha
pia tumetoa Dola za Kimarekani 500 ili kuweza kusaidia walemavu
mbalimbali katika kulejesha hali zao za kawaida hapa nchini” alisema Bw.
Al-Najem.
Aidha katika uzinduzi huo wa
Benki ya damu Balozi Al-Najem alijitolea damu unit moja ili kuweza
kuchangia benki hiyo ya taasisi ya Mifupa MOI ili kuweza kuhamasisjha na
wananchi wengine waweze kuchangia damu kwa msaada wa wagonjwa wengine.
Kwa upande wake Mkurugenzi
Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Lwezimula alisema kuwa katika
kuhakikisha Matibabu ya kibingwa yanapiga hatua nchini waliamu kuanzisha
kambi za matibabu kuanzia mwaka 2000 na kufanya taasisi zingine za afya
kuiga mfano huo.
“Tunataka kuhamasisha matibabu ya
kibingwa kufanyika nchini pamoja na uchangiaji damu kwani damu hiyo
haitatumika MOI peke yake bali hata kwenye Taasisi zingne na vituo vya
Afya nchini kote” alisema Dkt. Lwezimula.
Sambamba na tukio hilo Kikundi
cha Kutayarisha Madereva wa Magari Makubwa Wanawake (WOW) Afrika
Mashariki walijitolea kuchangia damu ili kuweza kusapoti benki hiyo kwa
ajili ya wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo ya damu.
“Tumehamasika kuja kuchangia damu
ili kuweza kutoa mfano kwa wanachi wengie waweze kujitolea katika
uchangiaji huu wa damu ili kujenga taifa lenye watu wenye afya bora”
alisema Mkurugenzi wa WOW Bw. Martin Gabone.









0 Comments