Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya
Wanging’ombe katika kikao kazi na watumishi hao chenye lengo la kuwasikiliza na
kutoa
ufafanuzi wa masuala ya kiutumishi.
Baadhi ya watumishi
wa Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe
wakimsikiliza
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean
Ndumbaro (hayupo pichani)
katika kikao kazi na watumishi hao chenye lengo kuwasikiliza na kutoa
ufafanuzi wa masuala ya kiutumishi
Waajiri nchini
wanatakiwa kuzingatia ufanisi wa utendaji kazi katika hatua za kuwapandisha
vyeo watumishi wa umma nchini.
Katibu Mkuu, Ofisi ya
Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro ametoa maelekezo
hayo akiwa katika kikao kazi na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya
Wanging’ombe.
Dkt. Ndumbaro amesema
lengo la Serikali ni kujenga ufanisi katika Utumishi wa Umma, hivyo suala la
upandishwaji vyeo Serikalini lazima lizingatie utendaji kazi wa watumishi wa
umma.
Katibu Mkuu Dkt. Ndumbaro amefafanua kuwa watumishi wa umma wakiajiriwa
pamoja haina watapandishwa cheo pamoja au muda wa kustaafu watakuwa katika cheo
kimoja, bali vyeo vitategemea utendaji kazi wao kati aliyefanya kazi kwa bidii
na ambaye hakuwajibika ipasavyo.
Dkt. Ndumbaro amesisitiza waajiri kuzingatia kigezo cha utendaji kazi
katika kuwapandisha vyeo watumishi wa umma ili kuimarisha utendaji kazi na
kuepuka kuwapandisha vyeo kiholela.
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
OFISI YA RAIS (UTUMISHI)
TAREHE 19 FEBRUARI, 2018



0 Comments