Random Posts

Mwalimu wa Sekondari Kufundisha Msingi sio Kushushwa Cheo

 Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro akisisitiza jambo kwa watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Makambako katika kikao kazi.
 Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro akiwa katika kikao kazi na watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Makambako.
 Sehemu ya watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Makambako walioshiriki kikao kazi na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro (hayupo pichani). Watumishi walipata fursa ya kuuliza masuala mbalimbali ya kiutendaji na kupewa ufafanuzi.
Mmoja wa watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Makambako akitumia fursa ya kuwasilisha hoja kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro (hayupo pichani) wakati wa  kikao kazi mjini Makambako.


Serikali kuwapangia baadhi ya walimu wa shule za sekondari kufundisha katika shule za msingi ni moja ya hatua katika kuongeza ufanisi na kuleta mgawanyo sawa wa walimu katika shule za sekondari na msingi.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro amesema hatua hiyo haimaanishi kuwa walimu wanaotoka katika shule ya sekondari kwenda kufundisha msingi wameshushwa cheo.

Dkt. Ndumbaro ametoa ufafanuzi huo katika kikao kazi na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mji wa Makambako. Amesisitiza kuwa lengo la Serikali ni kuondoa upungufu wa walimu katika shule za msingi na kuimarisha utoaji wa elimu.

Dkt. Ndumbaro ameainisha kuwa sifa za kufundisha na kiwango cha elimu zinaendana na mabadiliko yanayotokea duniani, hivyo mwalimu mwenye elimu ya kiwango cha Shahada ya kwanza kufundisha shule ya msingi isionekane ni jambo la ajabu.

Katibu Mkuu Dkt. Ndumbaro amewaambia watumishi wa umma maendeleo katika sekta yoyote, ikiwamo ya elimu yanakuja na mabadiliko hivyo wapokee mabadiliko na kufanya kazi ili kufikia lengo.

Florence Lawrence
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano

OFISI YA RAIS (UTUMISHI)
 20 Februari, 2018.

Post a Comment

0 Comments