Naibu Waziri wa Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mhe. Angeline Mabula, akizungumza na Waandishi
wa Habari wakati wa hafla fupi ya kugawa vifaa vya Samani kwa Mabaraza ya Ardhi
na Nyumba ya Wilaya, Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mhe. Angeline Mabula, akijaribu Kiti, moja ya
kifaa cha Samani, alivyokabidhi kwa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya;
Kulia kwake ni; Assessor Ramadhani (mwenye miwani), Mwenyekiti – Ilala; John
Bigambo na Mwenyekiti mwingine Ilala; Bi
Mwenda
Naibu Waziri wa Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mhe. Angeline Mabula, akimshika mkono Mwenyekiti
wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya ya Ilala; Mhe. Chenya kuashiria
Makabidhiano rasmi ya Samani kwa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya. Kulia
ni; Assessor Ramadhani (mwenye miwani), Mwenyekiti – Ilala; John Bigambo na
Mwenyekiti mwingine Ilala; Bi Mwenda
Naibu Waziri wa Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mhe. Angeline Mabula, akisisitizia kwa Wenyeviti
wa Mabaraza ya Ardhi, Nyumba na Wilaya wa Ilala na Kinondoni kuhusu Utendaji
bora wa kazi na umakini wa matumizi ya Samani alizokabidhi kwa Mabaraza ya
Ardhi na Nyumba ya Wilaya.
Na
Kitengo cha Mawasiliano
Wizara
ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Naibu Waziri wa Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Mhe. Angeline Mabula, amekabidhi vifaa vya
Samani kwenda kwenye Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya 12 nchini.
Makabidhiano ya Samani hizo,
ambapo jumla ya thamani yake ni Tsh. 112,923,404, vimenunuliwa na Mradi wa
maboresho ya Sekta ya Ardhi, ambao unatekelezwa kwa mkopo kutoka Benki ya
Dunia; Samani hizo ni pamoja na Meza,
Viti, Mabenchi, Kabineti, Shelfu na Kabati za kuhifadhi majalada ya kesi,
ambavyo vitaenda katika ofisi nane za
mabaraza ambazo ni Kinondoni, Moshi, Lindi, Kibaha, Dodoma, Tabora, Chato na
Musoma.
Akikabidhi samani hizo
jijini Dar es Salaam, Mhe. Mabula alisema Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya
ni miongoni mwa vyombo vilivyoundwa chini ya Kifungu cha 167 cha Sheria ya
Ardhi, sura ya 113 kwa ajili ya kusikiliza na kuamua mashauri yanayohusu
migogoro inayotokana na matumizi ya ardhi nchini.
Vilevile, uanzishwaji wa
Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya unazingatia Sheria ya Mahakama za Ardhi
sura ya 216 kifungu cha 22 kifungu kidogo cha kwanza (22 (1)).
Aidha, alisema Mabaraza ya
Ardhi na Nyumba ya Wilaya 53 yamekwisha kuanzishwa nchi nzima na yanafanya kazi
ya kusikiliza na kuamua mashauri ya migogoro inayotokana na matumizi mbalimbali
ya ardhi. Alisema;
“Nawakumbusha watumishi wote wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba
ya Wilaya kutimiza majukumu yao kwa weledi na kwa kuzingatia sheria, kanuni,
taratibu na miongozo iliyopo na itakayokuwa inatolewa ili kuboresha utoaji wa
huduma ya utatuzi wa migogoro itokanayo na matumizi ya ardhi”.
Aliendelea kusema kwamba
Idadi ya migogoro inayotokana na matumizi ya ardhi imeendelea kuongezeka siku
hadi siku;
“Napenda kuwakumbusha
wananchi kutumia huduma za Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya na kufuata
taratibu za utatuzi wa migogoro inayotokana na matumizi ya ardhi ili kupata
ufumbuzi wa migogoro hiyo kwa mujibu wa sheria”.
Alisema., na kuwakumbusha wananchi kutumia
Ofisi za Wasajili Wasidizi wa Mabaraza katika Kanda kwa ajili ya kutatua kero
zao kabla ya kuwasilisha kero hizo katika ngazi ya wizara.
Mabaraza ya Ardhi na Nyumba
ya Wilaya ni miongoni mwa vyombo vilivyoundwa chini ya Kifungu cha 167 cha
Sheria ya Ardhi, sura ya 113 kwa ajili ya kusikiliza na kuamua mashauri
yanayohusu migogoro inayotokana na matumizi ya ardhi nchini. Vilevile,
uanzishwaji wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya unazingatia Sheria ya
Mahakama za Ardhi sura ya 216 kifungu cha 22 kifungu kidogo cha kwanza (22
(1)).
0 Comments