Mwenyekiti
wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Mhe. Jason Rweikiza
(Mb) akimkabidhi Bi. Sabina Migayo Hati ya Hakimiliki ya Kimila wakati wa ziara
ya kikazi ya kamati hiyo yenye lengo la kukagua maendeleo ya miradi
inayotekelezwa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais - UTUMISHI na Utawala Bora, Kapteni (Mstaafu) Mhe. George H. Mkuchika (Mb)
akizungumza na wananchi wa kijiji cha Lunguya wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa yenye lengo la kukagua maendeleo ya
miradi inayotekelezwa na Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Baadhi
ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa wakipunga mikono kuwasalimu wananchi wa kijiji
cha Lunguya wilayani Kahama wakati wa
ziara ya kikazi ya kamati hiyo yenye lengo la kukagua maendeleo ya miradi.
Mratibu
wa MKURABITA Bi. Seraphia Mgembe (katikati ya umati) akizungumza
na wananchi wa kijiji cha Lunguya
wakati wa ziara ya kikazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali
za Mitaa yenye lengo la kukagua maendeleo ya mradi ya MKURABITA.
Baadhi
ya Wananchi wa kijiji cha
Lunguya wilayani Kahama wakimsikiliza
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Mhe.
Jason Rweikiza (Mb) wakati wa ziara ya kikazi ya kamati hiyo yenye lengo la
kukagua maendeleo ya miradi.
Mmoja
wa wanufaika wa Hati ya Hakimiliki ya Kimila wilayani Kahama akitoa shukrani
kwa Serikali kwa kitendo cha kutoa Hati za Hakimiliki za Kimila 275 kwa
wananchi wa vijiji vya Lunguya na Segese.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
SERIKALI YATOA HATI ZA HAKIMILIKI ZA KIMILA 275 KWA
WANANCHI WA MSALALA WILAYANI KAHAMA
Serikali kupitia
Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) mkoani Shinyanga imepima
mashamba 2158 na kutoa Hati za
Hakimiliki za Kimila 275 kwa
wananchi wa vijiji vya Lunguya na Segese wilayani Msalala.
Takwimu hizo za
urasimishaji zimetolewa Bw.Leonard M. Mabula kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala na Serikali za Mitaa kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halimashauri
ya Wilaya ya Msalala Bw. Simon Berege.
Akikabidhi Hati za
Hakimiliki za Kimila kwa baadhi ya wananchi, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Mhe. Jason Rweikiza (Mb) amewata wananchi
hao kuzitumia vizuri hati hizo ili waweze kujiondoa katika umasikini, kuboresha
familia zao na wilaya yao.
Miongoni mwa wananchi
waliopata fursa ya kukabidhiwa hati na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge
ya Utawala na Serikali za Mitaa ni Bw. Kimbuya Shija, Bw. Daudi Steven Ntowe,
Bw. Christopher Malajo, Bw. James Shija na Bi. Sabina Migayo.
Akizungumza na
wananchi katika kijiji cha Lunguya, Waziri mwenye dhamana ya usimazi wa Mpango
wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) nchini wa Ofisi ya Rais,
UTUMISHI na Utawala Bora, Kapteni (Mstaafu)
Mhe. George H. Mkuchika (Mb) amesema Serikali inarasimisha ardhi za wananchi wa
vijijini kuwa mali na kutoa hati za kimila zinazotambulika kwa mujibu wa sheria
kwa lengo la kuwawezesha kiuchumi wananchi wake.
Kapteni (Mstaafu) Mhe. Mkuchika,
amewahikishia wananchi kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe.
Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ina dhamira ya dhati ya kuboresha maisha ya
wananchi wenye kipato cha chini kupitia Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za
Wanyonge Tanzania (MKURABITA).
Naye, Mratibu wa Mpango
wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) Bi. Seraphia Mgembe amewata wananchi
kutumia hati za kimila kupata mitaji, ameongeza kuwa Serikali inatoa hati hizo
ili kuwawezesha wananchi wapate maendeleo kwa kutumia fursa hiyo kupata mitaji
kutoka katika taasisi za kifedha.
Akiwasilisha taarifa fupi ya utekelezaji kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala na Serikali za Mitaa, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab R. Telack
amefafanua kuwa, mradi umetekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala katika vijiji viwili (2) vya Lunguya na
Segese vilivyokuwa katika Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi ambapo jumla ya hati
za kimila 275 zimetolewa na MKURABITA.
Aidha, urasimishaji
katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kama ilivyo katika Halmashauri nyingine
nchini, umetoa matokeo chanya kwa kupunguza migogoro ya ardhi iliyokuwepo
na kuongeza usalama wa milki za ardhi za
wakulima waliorasimisha ardhi zao.
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
OFISI YA RAIS (UTUMISHI)
TAREHE 16 MACHI, 2018
0 Comments