Random Posts

Majambazi Wanne Wauawa kwa Kupigwa Risasi Kisarawe

 Kamanda wa polisi Mkoani Pwani,( ACP )Jonathan Shanna akionyesha silaha na vitu mbalimbali ,ikiwemo silaha ya kivita inayokaa na risasi 30 kwa wakati mmoja ,ambazo walizikamata katika gari walilolitumia majambazi waliofanya tukio la ujambazi wilayani Kisarawe  .(Picha na Mwamvua Mwinyi)
 Kamanda wa polisi Mkoani Pwani,( ACP )Jonathan Shanna akionyesha gari lililotumika kufanya ujambazi Kisarawe likiwa na plate no.bandia za kibalozi huku akiwa ameshika plate no.halisi zilizokuwa zimewekwa ndani ya gari hiyo .(picha na Mwamvua Mwinyi)
Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama Mkoani Pwani ambae pia ni mkuu wa Mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo ,akizungumzia tukio la ujambazi lililotokea Kisarawe na kudai Mkoa umejipanga kudhibiti wale wasioutakia mema Mkoa huo.
(Picha na Mwamvua Mwinyi)

Na Mwamvua Mwinyi,Kisarawe

MAJAMBAZI wanne wamefariki dunia baada ya kujibizana risasi na askari polisi ,wakati wakijaribu kufanya tukio la ujambazi katika nyumba ya mama Juliana Shirinde ambae ni mhasibu wa kikundi cha vikoba Ushelisheli,wilayani Kisarawe.

Aidha jeshi la polisi Mkoani Pwani,limenasa gari ndogo yenye namba za ubalozi ambayo waliiweka namba bandia T.17 CD 220 na kuifanyia ujambazi .

Akitoa taarifa ya tukio hilo ,kamanda wa polisi Mkoani humo, ( ACP) Jonathan Shanna ,alisema tukio hilo limetokea april 20 asubuhi saa 1:30  ,eneo la Kibaoni wilayani hapo.

Alieleza majambazi hayo yanasadikiwa yalikuwa matano wakitumia gari hilo,ambapo mmoja wao alishambuliwa risasi lakini alifanikiwa kutoweka .

Hata kamanda Shanna, alimtaka jambazi alietoweka kujisalimisha ndani ya masaa 24 .

Alieleza zipo tetesi zinazodaiwa baadhi ya waganga wa kienyeji ,ama matabibu ambao huchukua jukumu la kuwatibu majambazi waliojeruhiwa hivyo alitoa salamu kwao kuwa atakaebainika watamkamata na kumchukulia hatua kali za kisheria .

"Polisi ilipambana na majambazi watano ,kwa dhumuni la kupora fedha nyumbani kwa mama huyo mhasibu wa vicoba ambae alitoa fedha kwa ajili ya kugawia wanachama wenzie" alisema .

Kamanda Shanna alieleza kwamba ,katika mapambano hayo kikosi cha polisi kilishambulia majambazi wanne na mmoja alikimbia akiwa amejeruhiwa vibaya.

Alisema mbali ya hayo, walipopekua gari walikuta na kukamata silaha mbalimbali ikiwemo silaha ya kisasa ya kivita AK 67 inayotumia risasi 30 kwa wakati mmoja,magazine mbili , bunduki mbili na risasi 54 .

Pia walikamata pistol mbili bandia ,toy la umbile la kiume,na plate namba mbili zenye namba za usajali halisi , redio call plasta ngumu ya kuziba mdomo,kofia nyeusi ya kuficha macho na pingu .

Kamanda huyo alisema majambazi yasijaribu kufanya uhalifu kwani wapo vizuri kupambana na wahalifu .

Nae mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama Mkoani Pwani, mkuu wa Mkoa huo Evarist Ndikilo alisema Mkoa bado upo shwari kwani wapo vizuri kudhibiti uhalifu wowote utakaojitokeza.

Alimpongeza kamanda Shanna pamoja na askari polisi ambapo hakuna askari aliyepoteza Maisha.

"Kauli mbiu yetu ya mkoa ni Utaingia kwa hiari yako lakini hautotoka salama ,kwakuwa Mkoa huu ni wa Viwanda na uwekezazji tunahitaji amani na utulivu.

Ndikilo aliwahakikishia wawekezaji Mkoa wa Pwani upo salama na jeshi la polisi lipo tayari kulinda wananchi na mali zao .

Alisema wale ambao wana nia mbaya ya kukimbiza wenye nia ya kuwekeza wajue hawatafanikiwa .

Ndikilo alifafanua hakuna nafasi ya kufanya mambo ya ajabu ajabu na atakaethubutu atapata malipo anayoyahitaji.

Mganga mfawidhi wa hospital ya wilayani ya Kisarawe ,dokta Yona Kabata alikiri kupokea miili ya marehemu ya watu wanne kutoka kwa maafisa wa polisi,majira ya saa 4 :40 asubuhi April 20.

Post a Comment

0 Comments