Mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama, akizungumza
na wakazi waliokumbwa na adha ya nyumba zao kuzungukwa na maji
yaliyotokana na mvua zilizonyesha siku tatu mfululizo,kitongoji cha
Janga kata ya Janga.(Picha na Mwamvua Mwinyi)
Baadhi ya nyumba zilizozungukwa
na maji yaliyotokana na mvua zilizonyesha siku tatu mfululizo,kitongoji
cha Janga kata ya Janga.(Picha na Mwamvua Mwinyi)
Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha
NYUMBA
zaidi ya 30 zilizoko kwenye Kitongoji cha Janga, kata ya Janga wilaya
ya Kibaha ,mkoani Pwani zimezungukwa na maji, hali iliyosababisha wenye
nyumba hizo kuhama kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha mfululizo.
Akizungumza
na wakazi waliokumbwa na adha hiyo ,mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumpter
Mshama alisema wale ambao nyumba zao zipo jirani na bonde ,na zinaanza
kuingiliwa na maji waondoke kabla hayajaleta madhara .
Aidha alieleza wale ambao nyumba zao zilizo ndani ya maji watapewa viwanja bure.
"Mlioko
kwenye nyumba zaidi ya 30 zilizo kwenye maji na zinazokaribia
kuingiliwa na maji muondoke ili kuepukana na madhara yanayoweza
kujitokeza ikiwa ni pamoja na kupoteza maisha" alisisitiza.
Assumpter
alieleza, wakazi hao walijenga nyumba kwenye eneo hilo ambalo zamani
kulikuwa na bonde ambalo lilikuwa linalimwa mpunga na kuchimbwa kisima
kwa ajili ya maji.
"Gharama
za kutaka kujenga mfereji ni kubwa sana na serikali haina fedha za
kufanya hivyo njia pekee ni wakazi kuhama ili kuepusha maafa yanayoweza
kujitokeza kwani eneo hili halifai kuishi,"
"Ambao
nyumba ziko ndani ya maji watapatiwa viwanja bure sehemu nyingine
lakini watajenga wenyewe ,hawapaswi kuwepo hapo tena kwani hapafai
kuishi"
"Kwanza
hapa hamna hati za ujenzi wala za eneo hili na hapa hapajapimwa kwa
hiyo hapa so sehemu sahihi ya kuishi kwani maeneo yote yamepimwa laki
hapa hapajapimwa hivyo in vema mkaondoka," alifafanua Assumpter.
Diwani wa kata ya Janga, Chande Muhalika alisema ni tukio la kwanza kutokea kwenye bonde hilo .
Kwa mujibu wa diwani huyo ,zamani maji yalikuwa kidogo sana lakini safari hii maji yamekuwa mengi .
Nae
ofisa mtendaji wa Mji Mdogo wa Mlandizi Michael Mwakamo alisema kuwa
,baada ya kutokea hali hiyo waliwataka wananchi hao kuondoka ili
kuepusha madhara ambapo walioondoka na hakuna mwananchi aliyedhurika.
Nao
baadhi ya wakazi waliokumbwa na janga hilo ,akiwemo Luteni Kanali
mstaafu wa Jeshi Angolile Mwakajinga, Ramadhan Hemed, Sophia Matitu
walifafanua baada ya kuona maji yanaongezeka waliomba jeshini kambi ya
Ruvu Jkt mashine kwa ajili ya kuvutia maji lakini hawakufanikiwa.
Walibainisha
waliongea na wataalamu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha juu ya
uwezekano wa kuyatoa maji hayo wakasema njia pekee ni kuchimba mtaro
mkubwa na kuyapeleka maji hayo mto Mkalamo .
Hata hivyo gharama za kufanya hivyo zikaonekana kuwa kubwa.



0 Comments