Random Posts

Watumishi wa Umma 4,812 Kunufaika na Mafunzo Nchini China

 Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro  akifafanua jambo kuhusu  Watumishi wa Umma 4,812 watakaonufaika na fursa 659 za mafunzo ya muda mfupi na mrefu zilizotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa mwaka 2018.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro akizungumza na Waandishi wa Habari leo Ukumbi wa Idara ya Habari - Bunge kuhusu Watumishi wa Umma 4,812 kunufaika na fursa 659 za mafunzo ya muda mfupi na mrefu zilizotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa mwaka 2018.


Watumishi wa Umma 4,812 kunufaika na fursa 659 za mafunzo ya muda mfupi na mrefu zilizotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa mwaka 2018.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro amesema hayo leo wakati wa kikao na Waandishi wa Habari kilichofanya ukumbi wa Idara ya Habari-Bunge mjini Dodoma.

Dkt. Ndumbaro ameainisha kuwa, mafunzo hayo yamelenga katika eneo la Uhandisi wa Viwanda, Mawasiliano na Usafirishaji, Kilimo, Elimu, Afya, Biashara na Uchumi, TEHAMA na Utawala Bora ambayo ndio maeneo ya kipaumbele katika Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa miaka mitano (2016/17 hadi 2020/21).

Dkt. Ndumbaro ametoa wito kwa Watumishi wa Umma kuchangamkia fursa hizo ambazo zitawajengea uwezo wa kiutendaji katika kutoa huduma kwa umma.

Dkt. Ndumbaro ametoa wito kwa waajiri kuwawezesha watumishi walio chini yao kuhudhuria mafunzo hayo kwa mujibu wa Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo ya Utumishi wa Umma iliyopo kwa kuzingatia mipango ya mafunzo.

Akitoa shukrani kwa niaba ya Serikali, Dkt. Ndumbaro ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa kutoa fursa hizo. Aidha, amewashukuru na wadau wengine wa maendeleo ambao ni India, Australia, Japani, Jamhuri ya Korea, Singapore, Misri na Uholanzi kwa kushirikiana na Serikali kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa Umma nchini kwa kutoa fursa za mafunzo 1,865 kati ya mwaka 2015/16 na 2017/18.

Fursa hizo zinapatikana kupitia tovuti ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (www.utumishi.go.tz).

IMETOLEWA NA:
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
OFISI YA RAIS (UTUMISHI)
TAREHE 17 APRILI, 2018

Post a Comment

0 Comments