Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Kale wa Serikali
ya Kifalme ya Oman Bwana Salum Mohamed Al-Mahrooqi kulia aliyevaa kilemba
akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Vuga
Mjini Zanzibar.
.Bwana Salum Mohamed Al- Mahrooqi aliyenyanyua
Mkono akielezea mikakati ya Oman katika kuendeleza Uhusiano na Zanzibar wakati
akizungumza na Balozi Seif Ali Iddi wa kwanza kutoka Kulia.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif
wa kwanza Kutoka Kulia akiishukuru Serikali ya Oman kwa misaada inayoendelea
kutoa kwa Zanzibar.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Kale wa Serikali yaÂ
Kifalme ya Oman Bwana Salum Mohamed Al- Mahrooqi aliyevaa Kilemba akifafanua
jambo mara baada ya kumaliza mazungumzo yao na Balozi Seif.
Kushoto ya Bwana Salum Mohamed Al-Mahrooqi ni Waziri wa Habari,
Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mh. Mahmoud Thabit Kombo na kulia ya Balozi
Seif ni Waziri Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mohamed
Aboud Mohamed.
.......................................................
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Kale wa Serikali ya Kifalme
ya Oman Bwana Salum Mohamed Al-Mahrooqi alisema uwepo wa Jumla la Ajabu liliopo
Forodhani Mji Mkongwe maarufu 'Beit Al Ajaib' utaendelea kuwa utambulisho wa
Zanzibar Kimataifa katika masuala ya Kihistoria na Utamaduni.
Alisema Jengo hilo Maarufu ndani ya ukanda wa Afrika Mashariki
na Dunia tokea Karne ya 17 linastahiki kufanyiwa ukarabati makubwa ili
kulirejeshea hadhi yake ya kawaida na Oman tayari imeahidi kugharamia ukarabati
hayo.
Bwana Salum Mohamed Al-Mahrooqi aliyeambatana na Balozi Mdogo wa
Oman aliyepo Zanzibar Bwana Ahmad
Hamoud Al Habsy alisema hayo wakati wa mazungumzo yake
na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ofisini kwake Vuga
Mjini Zanzibar.
Katibu Mkuu Salum alisema hatua ya Serikali ya Oman kuahidi
kutoa gharama za ukarabati ya Jumba hilo imekuja kutokana na Historia kubwa ya
Uhusiano uliopo kati ya Zanzibar na Oman kwa Karne kadhaa zilizopita.
Alisema Historia ya pande hizo mbili zenye udugu wa Damu hasa
katika masuala ya Utamaduni utaendelea kuwepo na kuimarishwa kwa faida ya
Vizazi vya sasa na vile vitakavyokuja hapo baadae.
Katibu Mkuu huyo wa Wizara ya Mambo ya Kale wa Oman alimueleza
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba ziara ya Ujumbe wake
Visiwani Zanzibar umekusudia kufanya uratibu wa ushirikiano wa mambo kadhaa
yatakayowezesha kusaidia na kuimarisha ushirikiano wa pande hizo mbili.
Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi
Seif Ali Iddi alisema Zanzibar bado ni tulivu na kuwaomba Waoman
kutumia fursa iliyopo ya Zanzibar ni Njema kufika kujifunza mambo tofauti
ya Kihistoria ambayo yana mafungamano ya Oman.
Balozi Seif aliuhakikishia Ujumbe huo wa Oman kwamba
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kutoa ushirikiano kwa ndugu zao wa
Oman na kusema kwamba, wasimamizi pamoja na wajenzi wa ukarabati huo wa Jumba
la Beit Al Ajaib watepewa msaada wa kina katika kuona kazi hiyo inafanyika na
kumalizika kwa mafanikio makubwa.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisisitiza kwa kutoa mfano,
kwamba mambo yaliyopo Zanzibar yenye mafungamano na uhusiano na Oman ni Majengo
ya Kihistoria yaliyopo Mji Mkongwe ambayo yataendelea kutunzwa ili yabaki kuwa
kumbukumbu nzuri ya kukuza ushirikiano wa pande hizo mbili.
Katibu Mkuu huyo wa Wizara ya Mambo ya Kale wa Oman Bwana Salum
Mohamed Al- Mahrooqi na Ujumbe walitembelea sehemu mbali mbali za Kihistoria,
maeneo ya mashamba ya Viungo pamoja na kukutana na Viongozi mbali mbali
wanaohusika na masuala ya Mambo ya Kale.
Picha na habari Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwa
Kushirikiana na
Idara ya Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Afrika Mashariki Ofisi ya
Zanzibar




0 Comments