Diwani kata ya Visiga ,Kambi Legeza akizungumza jambo kuhusiana na sekta ya elimu kwa wakazi wa Visiga.
Wakazi wa kata ya Visiga wakimsikiliza Diwani wa kata ya Visiga ,Kambi Legeza hayupo pichani.
(Picha na Mwamvua Mwinyi)
Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha
WANAFUNZI
wa shule ya Msingi Visiga,Kibaha mkoani Pwani wanakabiliwa na
changamoto ya mlundikano madarasani kutokana na upungufu wa vyumba vya
madarasa 30 na madawati hali inayosababisha baadhi yao kukaa chini.
Aidha kila darasa kuna idadi ya wanafunzi 170 suala ambalo ndilo linalosababisha uhaba wa madawati na mlundikano huo.
Akielezea
tatizo hilo katika mkutano wa wazazi na wananchi, diwani wa kata ya
Visiga, Kambi Legeza alisema changamoto zimekuwa kubwa kutokana na
mwitikio mkubwa wa wazazi kupeleka watoto wao shule, kwa kuunga mkono
agizo la serikali la elimu bila malipo .
Alieleza
moja ya shule kwenye kata hiyo inayokabiliwa na changamoto hiyo ni
shule ya Msingi Visiga ambayo ndiyo shule kubwa na yenye wanafunzi wengi
kwenye kata hiyo.
Legeza
alisema ,changamoto hiyo imeisukuma na kuulazimu uongozi wa kata hiyo
,kuitisha mkutano huo wa wananchi ambao umeridhia kila kaya kuchangia
kiasi cha sh.4,000 ili kupunguza changamoto zilizopo kwenye shule za
kata ya Visiga ikiwemo shule hiyo.
“Tumekubaliana
kila kaya ichangie kiasi hicho kwa ajili ya kuondoa changamoto za
vyumba vya madarasa , upungufu wa madawati na matundu ya vyoo ”
“Suala
la kuchangia maendeleo ya elimu siyo kosa tatizo watu wanashindwa
kuelewa michango mashuleni ndiyo imekatazwa lakini wananchi
hawajakatazwa kuchangia kwa hiari yao kuondoa changamoto zilizopo ”
alisema diwani huyo .
Hata
hivyo ,Legeza alielezea jukumu la kutatua changamoto za kielimu ama
maendeleo ya kijamii ni la jamii yenyewe badala ya kuitegemea serikali
pekee.
Alisema
kwasasa ,watafuata taratibu za kuomba kibali halmashauri na wilaya na
fedha za mchango huo zote zitaingizwa kwenye mfuko wa elimu wa
Halmashauri.
Nae
mwenyekiti wa kamati ya shule ya msingi Visiga Moshi Mnaki alisema,
changamoto za uhaba wa madarasa inasababisha wanafunzi kusoma kwenye
mazingira magumu.
Alisema
yapo madarasa mawili kongwe yaliyojengwa mwaka 1983 ambayo wanahitaji
kuyakarabati na inatakiwa mil. Tisa ili kukamilisha ukarabati huo.
Mnaki alisema, darasa moja linafikia wanafunzi 170 ikiwa na idadi ya wanafunzi 1,350.
Mnaki alisema vyumba vya madarasa vilivyopo 11 mahitaji yakiwa ni 30 .
Changamoto nyingine ni upungufu wa matundu ya vyoo, ambapo mahitaji yake ni 53 na vilivyopo 28 ,mapungufu 25.
Mnaki
alielezea, madawati mahitaji 395 yaliyopo 317 ,upungufu 78 ,meza za
walimu mahitaji 34 ,zilizopo 9 ,pungufu 29 ,viti mahitaji ni 34, na
vilivyopo 19.
Mkazi wa Visiga ,Saidi Mtende alisema wamekubaliana kuchangia 4,000 kuondoa changamoto za kielimu .
Alisema
,wazazi wasikumbatie watoto wao na kuwageuza mabwana wakubwa kwa
kuwaacha majumbani pasipo kuwapeleka mashuleni kupata elimu .


0 Comments