Kaimu msajili wa bodi ya AQRB, Albert Munuo akizungumza na wabunifu,
wakadiriaji majenzi na wadau mbalimbali wa sekta ya ujenzi wakati wa mafunzo endelevu ya kuwajengea uwezo katika sekta hiyo.
Wadau wa sekta ya ujenzi wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Picha ya pamoja.
Habari Picha/ na Philemon Solomon
.........................................
BODI ya Usajili wa Wabunifu na Wakadiriaji Majenzi AQRB
imesema migogoro katika sekta ya ujenzi inasababisha miradi mingi
kutokamilika kwa wakati sambamba na kuwezesha kushindwa kujua thamani
halisi ya ujenzi.
Akizungumza
na waandishi wa habari mara baada kumalizika kwa mafunzo yaliyoandaliwa
na AQRB na kuwakutanisha wabunifu, wakadiriaji majenzi na
wadau mbalimbali wa sekta ya ujenzi mwishoni mwa wiki Kaimu msajili wa bodi
hiyo Albert Munuo alisema mafunzo haya ni muendelezo wa taratibu zao ambapo
wataalamu wamekuwa wakikutana mara mbili kwa mwaka na kujadili mada mbalimbali.
"
Leo tumejadili migogoro mbali mbali ambayo hujitokeza katika sekta ya ujenzi na
athari zake ambapo tumebaini kwamba migogoro hiyo mbali na kusababisha
gharama za ujenzi kuwa juu pia imekuwa ikisababisha miradi mingi kushindwa
kukamilika kwa wakati,'"alisema Munuo.
Alizitaja
sababu zinazosababisha migogoro katika sekta ya ujenzi kuwa ni pamoja na
kutokamilika kwa nyaraka za ujenzi kikamilifu ikiwepo michoro sambamba na
mwenye mradi kutomlipa mkandarasi na mtaalamu mshauri kwa wakati.
Alisema
yapo matatizo mengine ambayo husababishwa na washauri wasimamizi kwa kushindwa
kutoa maelekezo ya kitaalamu kwa wakati kwa mkandarasi.
'
Kwa kuzingatia mjadala wote wataalamu tuliokutana tumeona ipo haja kila mtu
kutimiza majukumu yake ili kuondoa migongano na kwa hili ni lazima hatua za
kisheria zichukuliwe kwa wataalamu watakaoenda kinyume cha
taratibu,"alisisitiza Mumuo
Akizungumzia
uhaba wa wataalamu wa fani ya ubunifu na ukadiriaji majenzi alisema hauendani
na uhitaji na kwamba kwa sasa wanaotambulika ni 1,500 tu.
Alisema
kutokana na hali hiyo AQRB imekuwa ikihamasisha vijana kupitia programu maalumu
ambapo wataalamu wamekuwa wakipita mashuleni kuanzia shule za sekondari
kuhamasisha wanafunzi kusoma masomo ya sayansi ili baadae waweze kusoma fani
hii na kulipunguzia taifa uhaba wa wataalamu hao.
Pia
alisema ili kuondoa mkanganyiko uliopo baina ya wataalamu wa
ubunifu,wakadiriaji majenzi na wahandisi wameandaa mpango mkakati maalumu
wa kuielima jamii utofauti wa majukumu ya wataalamu hao huku akihimiza kuwataka
watanzania kubadilika na kuwatumia wataalamu katika ujenzi mbalimbali ili
kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na kukosa ushauri kutoka kwa
wataalamu hao.
Hata
hivyo Munuo aliwaomba wataalamu wenye makampuni kuwachukua vijana wanaotoka
vyuoni na kuwapa kazi ili waweze kupata uzoefu wa fani walizosomea.
Naye
mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo ambaye aliwasilisha mada inayohusu jinsi ya
kuzuia migogoro ya sekta ya ujenzi Wakili Madeline Kimei aliunga mkomo suala la
vijana wanaotoka vyuoni kupewa kazi na wenye makampuni kwa kusema kuwa kupatiwa
kazi kwa vijana hao kutawahamasisha na kuwapa uzoefu wa kazi.



