Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo
na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) Ludigija Bulamile, (kulia) akizungumza na
waandishi wa habari (hawapo pichani) ofisini kwake Jijini Dar es Salaam jana
kuhusina na maandalizi semina endelevu ya kuwanoa watalaam wa sekta ya ujenzi itakayofanyika Novemba 22-23
mwaka huu Dar es Salaam (kushoto) Kaimu Msajili wa Bodi hiyo Albert Munuo.
PICHA NA PHILEMON SOLOMON
Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu
Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) Ludigija Bulamile, (katikati) akizungumza
na waandishi wa habari (hawapo pichani) ofisini kwake Jijini Dar es Salaam jana
kuhusina na maandalizi kufanyika kwa semina ya kuwanoa watalaam wa sekta ya ujenzi itakayofanyika Novemba 22-23
mwaka huu Dar es Salaam (kushoto) Kaimu Msajili wa Bodi hiyo Albert Munuo,
kulia Kaimu Msaidizi wa Msajili Fedha na Utawala, Mariam Chiponde. PICHA NA
PHILEMON SOLOMON
Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu
Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) Ludigija Bulamile akijibu maswali kwa
waandishi wa habari. PICHA NA PHILEMON SOLOMON
Kaimu Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo
na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) Albert Munuo (aliyevaa miwani) akifafanua
kuhusina na semina hiyo. PICHA NA PHILEMON SOLOMON
Na Philemon Solomon
WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe,Novemba 22 anatarajia kufungua semina ya kuwanoa Wabunifu Majengo, Wakadiriaji
Majenzi na wataalamu wengine wanaoshabihiana
katika sekta ya ujenzi ili kukabiliana na mabadiliko ya sayansi na
teknolojia katika sekta ya ujenzi.
Akizungumza na waandishi wa
habari Dar es Salaam jana Kaimu Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo
na Wakadiriaji Majenzi (AQRB) Albert Munuo alisema mada mbalimbali zinazohusu
matumizi bora ya nishati katika majengo zitajadiliwa.
Alisema pamoja na majukumu
mengine yaliyoainishwa katika kifungu cha 5 cha sheria namba 4/2010 bodi ina
jukumu la kuratibu na kutoa nafasi za mafunzo endelevu kwa wadau wa sekta ya
ujenzi kupitia warsha na semina mbalimbali ili kuhakikisha wataalamu wanaendana
na maendeleo ya teknolojia katika kutoa huduma bora kwa jamii.
"Semikna hii ya Novemba 22
ni moja ya semina endelevu zinazotolewa na Bodi kwa wataalamu ambapo mada mbalimbali zinazohusu
matumiz bora ya nishati katika majengo,nyumba za gharama nafuu,ushindani wa
kazi za kitaalamu katika soko la jumuiya ya Afrika Mashariki na ubunifu zitajadiliwa,"alisema
Munuo na kuongeza kuwa wataalamu wataweza kubadilishana uzoefu wa kazi za kitaalamu
kwa lengo la kuziborsha.
Pia alisema wataalamu watapata
fursa ya kupata nasaha kutoka kwa viongozi mbalimbali wa serikali huku akisisitiza
kwa kuwataka Wabunifu Majengo,Wakadiriaji Majenzi,Wahandisi,Wakandarasi na
wadau wengine kujitokeza kushiriki katika semina hii ili kuwaongezea ujuzi na maarifa
ya kuboresha utendaji kazi wao.
Aidha Bodi inawaomba waajiri
wote wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi sambamba na wataamu
wanaoshabihiana nao kuwafadhili kwa kuwalipia ada ya ushiriki watumishi wao na
kuwaruhusu kushiriki ili waweze kuongeza tija katika utendaji kazi wao.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa
Bodi hiyo Ludigija Bulamile aliongeza kuwa, semina hizi ni muendelezo wa semina
ambazo zilianza mwaka 2003 na hufanyika mara mbili kwa mwaka ambapo jumla ya
wadau 6,403 wa sekta ya ujenzi wameweza kunufaika na mafunzo haya.
Bulamile aliongeza kwa
kuipongeza serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na rais Dkt. John Magufuli kwa
kutambua umuhimu wao na kuwashirikisha katika shughuli mbaklimbali za miradi
ianyoendelea ukiwepo ule wa ujenzi wa reli ya kisasa SGR.
"Katika kipindi cha miaka
mitatu ya rais Dkt. Mgufuli serikali imeendelea kuwatambua wataalamu wetu na kuwashirikisha
katika mkradi mbalimbali ukiwepo wa ujenzi wa reli ya kisasa,"alisema
Buhamile na kuongeza kusisitiza kuwataka watanzania kuwatumia waalamu hao katika
ujenzi ili waweze kujenga nyumba bora zenye kuzimgatia vipato vyao.
Hata hivyo aliwaasa kuachana na
dhana potofu kuwa wataalamu hao wamekuwa wakitumia harama kubwa kutoa ushauri
kwa jamii kitua mbapo si cha kweli badala yake watambue kuwa wataalamu hao ni
watu ambao wanarahisisha maisha kwa kshauri ujenzi kulingana na vipato vya
jamii.





0 Comments