SEMINA ENDELEVU YA CPD KUFANYIKA MKOANI MWANZA DESEMBA 2, 3 MWAKA HUU - MTAZAMO MEDIA

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, 25 November 2021

SEMINA ENDELEVU YA CPD KUFANYIKA MKOANI MWANZA DESEMBA 2, 3 MWAKA HUU

Msajili wa Bodi ya Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi Arch.Edwin Nnunduma ( wakwanza kulia) akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa ya mafunzo endelevu ya CPD yatakayofanyika mkoani Mwanza Desemba 2 na 3 Mwaka huu, katikati ni  Msajili Msaidizi  wa Usajili na Mafunzo wa Bodi hiyo QS. Bundala Mashaka Robaert na Mkuu wa Utawala na Fedha. Bi Mariam Chipunde.

Msajili wa Bodi ya Wabunifu majengo na Wakadiriaji Majenzi Arch.Edwin Nnunduma ( katikati) akiendelea kuzungumza na waandishi wa habari.

Msajili wa Bodi ya Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi Arch.Edwin Nnunduma akijibu maswali kutoka kwa waandishi wa habari.

HABARI PICHA / NA PHILEMON SOLOMON

......................................................

Bodi ya Wabunifu wa Majengo  na Wakadiriaji Majenzi ( AQRB) imeishauri jamii kutumia wataalamu wa ujenzi waliosajiliwa ili kusaidia miradi ya ujenzi kudumu kwa muda mrefu nakwamba hali  hiyo inasaidia kupunguza gharama za ujenzi .


Ushauri huo umetolewa na Arch.Msajiri wa Bodi hiyo Edwini Nnunduma wakati akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa ya mafunzo endelevu ya CPD yatakayofanyika mkoani Mwanza Desemba 2 na 3 Mwaka huu huku Mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Gabriel Robert.


Arch.Nnunduma  amesema kwamba  baadhi ya Jamii imekua ikitumia mafundi waliosomea katika vyuo vya ufundi mbalimbali kama vile VETA  katika kufanya shughuli za ujenzi bila kutumia wataalamu wa ujenzi waliosajiliwa na bodi hiyo hali ambayo amesema inachangia majengo mengi kutokua na ubora.


“Sisi tunasisitiza wataalamu wetu watumike hata katika kazi binafsi,inasaidia kufahamu ghamara za ujenzi kabla ujenzi hujaanza kufanyika,lakini pia inasaidia kujenga nyumba zenye ubora  kulingana na uwezo wa mtu kiuchumi”amesema Arch.Nnunduma.


Kuhusu semina ya mafunzo endelevu Nnunduma amesema kwamba Semina hiyo inatarajiwa kuwa na washiriki wapatao 250 hadi 300 ambao ni wataalamu katika sekta tofauti ikiwemo Wabunifu wa Majengo,Wakadiriaji wa Majenzi,Wasimamizi wa Majengo,Wasimamizi wa Miradi na Wasamabazaji wa Vifaa vya Ujenzi.


Aidha amesema kuwa mada mbalimbali zitajadiliwa ,ikiwemo mada kuhusu sheria mpya ya Kodi kwenye Sekta ya Ujenzi ambapo wataalamu hao watafundishwa namna ya kupeleka mapato TRA kwa njia ya kielektroniki kutokana na mabadiliko ya kisayansi na  teknolojia.


Kwa upande wake Msajili Msaidizi  wa Usajili na Mafunzo wa Bodi hiyo Bundala Mashaka Robaert amewaomba washiriki wajitokeze kwa wingi kushiriki semina hiyo waweze kujengewa uelewa kuhusu mabadiliko ya teknolojia yaliyopo kwa sasa.


“Washiriki wajitokeze kwa wingi,makampuni binafsi yawawezeshe wataalamu waweze kushiriki semina hii ni muhimu sana manake mada ambazo tunaenda kuzijadili zitatusaidia sana katika utendaji wetu wa kazi ,pia semina hii hufanyika mara mbili tu kwa mwaka “amesema Msajili huyo Msaidizi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages