Monday 26 June 2023

Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ahutubia katika Maadhimisho ya Kitaifa ya Kupiga Vita Matumizi na Biashara ya Dawa za Kulevya Duniani, Mkoani Arusha

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali pamoja na Wananchi katika Maadhimisho ya Kitaifa ya Kupiga Vita Matumizi na Biashara ya Dawa za Kulevya Duniani ambayo Kitaifa yamefanyika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha tarehe 25 Juni, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya Kutambua Mchango wake kwenye Mapambano dhidi ya dawa za Kulevya nchini kutoka kwa Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa aliyeiwasilisha kwa niaba ya Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) katika Maadhimisho ya Kitaifa ya Kupiga Vita Matumizi na Biashara ya Dawa za Kulevya Duniani ambayo Kitaifa yamefanyika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha tarehe 25 Juni, 2023.

PICHA NA IKULU

No comments:

Post a Comment