Monday 26 June 2023

Wataalamu wa Sekta ya Ujenzi Watakiwa Kuzingatia Sheria za Kodi.

Katibu Tawala Msaidizi,Miundombinu wa Mkoa  wa Morogoro  Mhandisi  Ezron Kilamham akitoa hotuba wakati akifungua semina ya mafunzo endelevu ya (CPD) yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Nshera Hoteli Mjini Morogoro.
.............................
PICHA ZOTE NA SOLOMON PHILEMON -MOROGORO
Baadhi ya wataalamu wa Majenzi wakiwa kwenye mafunzo endelevu ya wataalamu wa Majenzi yaliyoandaliwa na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi  (AQRB) mjini Morogoro.

Katibu Tawala Msaidizi,Miundombinu wa Mkoa  wa Morogoro  Mhandisi  Ezron Kilamhama akisalimiana na Kaimu Msajili wa Bodi ya AQRB  Mkadiriaji Majenzi Qs. Nyaswa Kalomo aliopowasili kufungua mafunzo endelevu ya wataalamu wa Majenzi yaliyoandaliwa na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi  (AQRB) mjini Morogoro ( kulia ) Msajili Msaidizi (Usajili na Mafunzo) wa Bodi hiyo Qs. Mashaka Bundala, Mwenyekiti wa Bodi hiyo Arch. Dkt. Ludigija Bulamile.

Mwenyekiti wa Bodi hiyo Arch. Dkt. Ludigija Bulamile akizungumza.
Kaimu Msajili  Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi  (AQRB) Qs. Nyaswa Kalomo akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Viongozi wakiwa meza kuu.
Baadhi ya wataalamu wa Majenzi wakiwa kwenye mafunzo endelevu ya wataalamu wa Majenzi yaliyoandaliwa na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi  (AQRB) mjini Morogoro.
Msajili Msaidizi (Usajili na Mafunzo) wa  Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi  (AQRB) Qs. Mashaka Bundala akisisitiza jambo wakati akitoa neno la shukrani.
.......................

 Katibu Tawala Msaidizi,Miundombinu Mkoa wa Morogoro  Mhandisi  Ezron Kilamhama.
...............................................

SERIKALI imeziagiza Bodi zenye Mamlaka ya Usimamizi katika Sekta ya Ujenzi kuhakikisha wataalamu  wanaopewa dhamana ya kutekeleza miradi ya Ujenzi wanazingatia sheria za Kodi  Ili serikali iweze kupata mapato na Shughuli za ujenzi ziendelee kutoa mchango  katika ukuaji wa uchumi

Akifungua mafunzo endelevu ya wataalamu wa Majenzi yaliyoandaliwa na Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi  (AQRB) mjini Morogoro Katibu Tawala Msaidizi,Miundombinu wa Mkoa  huo Mhandisi  Ezron Kilamhama kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa  alisema  katika baadhi ya miradi ya Ujenzi inayosimamiwa na kutekelezwa na wataalamu wa ndani ukwepaji wa kodi umekuwa mkubwa kiasi cha kusababisha malalamiko dhidi ya umahiri na ujuzi wa Kampuni za ndani

Alisema kaguzi ambazo zimekuwa zikifanywa  na mamlaka za Usimamizi kwenye miradi yetu zimekuwa na mapungufu makubwa kwenye ubora  na gharama za miradi kuwa juu.

"Nimefurahia sana kusikia katika mafunzo haya kutakuwa na mada ya Mapitio kuhusu uzingatiaji wa masuala ya Kodi, mada hii itukumbushe uwajibikaji, ufuatiliaji na uzingatiaji  wa nidhamu ya kulipa Kodi katika kuendeleza Sekta ya Ujenzi," Alisisitiza  Mhandisi Kilamhama

Aliongeza kuwa, kuhusu mada ya ulinganifu wa gharama za ushauri kwa mujibu wa sheria ya AQRB na ya PPRA mada hii itadaidia kupata uelewa wa pamoja Juu ya ukokotoaji wa ada za ushauri kwa kutumia sheria hizi mbili za AQRB na PPRA

Pia alisema kwenye mada ya Usimamizi wa  miradi katika Tasnia ya Ujenzi Nchini Tanzania mada hii ni muhimu hasa wakati huu ambapo serikali na Sekta binafsi zinatekekeza miradi mingi  ya Ujenzi ambayo imekuwa kichocheo Cha ukuaji wa uchumi Nchini

"Bila wataalamu wetu kusimania vyema miradi hii hatutaweza kupata matokeo yanayoendana na thamani ya uwekezaji unaofanywa na serikali  kwa kushirikiana na Sekta binafsi,"alisema Mhandisi  Kilamhama

Akifafanua kuhusiana na

Changamoto mbalimbali zinazoikabili swkta hiyo ikiwemo ya baadhi ya Taasisi za umma zinavyotekekeza miradi  ya Ujenzi kwa utaratibu wa kutumia wataalamu wa ndani ya Taasisi yaani 'Force Accaunt' isivyo sahihi serikali imeliona suala Hilo na kila mara  viongozi wakuu wa serikali  wamekuwa wakitolea maelekezo  kuwa sheria ya ununuzi wa umma  inayohutaji wataalamu watumike uzingatiwe

Alisema serikali itaendelea kushirikisha kikamilifu wataalamu wa ndani katika hatua zote za ujenzi katika miradi ya Ofisi za halmashauri na Manispaa,Majengo ya hospitali za Rufaa,Mkoa na Kanda pia Masoko makubwa ya Kusasa na miradi ya Ujenzi wa vitui vikubwa Vya mabasi ya masafa marefu unatekekezwa kwa kutumia wataalamu waliosajiliwa na bodi

Kwa upande wake Kaimu Msajili wa Bodi ya AQRB  Mkadiriaji Majenzi Nyaswa Kalomo kwa niaba ya Msajili wa Bodi hiyo aliiomba  Serikali kuendelea kuajiri wataalamu waliosajiliwa na bodi katika  ofisi zote za umma Ili kutoa miongozo ya ujenzi kwa waendelezaji wa Majengo waliopo mjini na vijijini

Alisema idadi ndogo ya Wabunifu Majengo, wakadiriaji Majenzi, Wabunifu madhari na wataalamu wengine wa ujenzi unachangia kwa kiasi kikubwa taifa katika ushiriki wa miradi mbalimbali

"Kukosekana kwa sheria ya Majengo ,sheria hii Ina nanufaa mengi kwenye Tasnia ya Majengo sambamba na wataalamu kuhusika moja kwa moja kupanga,kubuni, kujenga na kutunza Majengo na mazingira kwa kuzingatia usalama na afya ya watu na Mali, kudhibiti ubora wa vifaa Vya Ujenzi matumizi Bora ya mifumo na miundombinu ya Maji, gesi, nishati, mwanga, upepo, joto na baridi ndani na nje ya jengo pamoja na kutunza mazingira

Naye Mwenyekiti wa Bodi hiyo Dkt. Ludigija Bulamile alisema mafunzo haya kwa wataalamu wa ujenzi ni muendelezo wa taratibu za Bodi ya AQRB katika kuwanoa wataalamu Ili kuwawezesha kupendana na mabadiliko ya teknolojia ya Ujenzi

"Uchaguzi wa mada umefanywa mahususi  Ili kuwakumbusha wataalamu wetu umuhimu wa kusimaia miradi ya Majengo na mazingira katika utekelezaji wa kazi zao za kila siku,"alisema Dkt Ludigija na kuongeza kuwa  mafunzo hayo ni Usimamizi wa Miradi katika Tasnia ya Ujenzi Tanzania ambayo utajadiliwa pamoja na mada ndogo zingine nne

Hata hivyo alizitaja mada zingine zitakazo jadiliwa kwenye mafunzo hayo kuwa ni pamoja na shugulikia madai na masuluhisho ya migogoro katika Tasnia ya Ujenzi Nchini,Mapitio kuhusu uzingatiaji wa masuala ya Kodi na ulinganifu wa gharama za ushauri kwa mujibu wa sheria ya AQRB na PPRA.

No comments:

Post a Comment