Wednesday 23 August 2023

KAMPUNI YA JOSTANO TRANS KINARA SEKTA YA USAFIRISHAJI NCHINI

Mabasi ya Kampuni ya Jostano and General Supplises Limited yakiwa Stendi ya Mabasi ya Mkoa wa Singida Misuna tayari kwa safari zake.

.....................................................

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam

KAMPUNI ya Jostano and General Supplises Limited licha ya kuanza kufanya kazi  hivi karibuni imekuwa kinara katika sekta ya usafirishaji hapa nchini hususani katika Mikoa ya Singida, Manyara, Morogoro, Dar es Salaam, Dodoma na Mbeya.

Licha ya kuwa na miaka miwili katika sekta hiyo tangu ianze kufanya kazi zake mwaka 2021 kampuni hiyo imejizolea umaarufu mkubwa kutokana na utoaji wa huduma zake kwa viwango vya hali ya  juu na kuwa kimbilio la abiria wengi.

Mfanyabiashara Margaret Ntandu ambaye anasafirisha mchele kati ya Mkoa wa Tabora kupitia Singida anasema amekuwa akisafirisha bidhaa hiyo kupitia mabasi ya kampuni hiyo na haja wahi kupata changamoto yoyote.

'' Nimekuwa nikisafirisha mizigo yangu kutoka Singida kwenda Dodoma sijawahi kupata changamoto ya aina yoyote iwe ya kupotea mzigo na nyingine na hata bei zao ni rafiki ukilinganisha na mabasi ya kampuni zingine,'' alisema Ntandu.

Edina Alex ambaye ni mfanyabiashara wa vitenge anayevitoa Tunduma na kuvipeleka Singida anasema mabasi ya kampuni hiyo ndiyo anayopanda wakati akifuata bidhaa zake hizo na kuwa wafanyakazi wa kampuni hiyo wamekuwa na lugha nzuri kwa abiria.

Alex anasema tangu kampuni hiyo ianze kufanya safari zake Mkoa wa Mbeya anatumia mabasi ya kampuni hiyo na akaupongeza uongozi kwa kusimamia vizuri utendaji kazi wa wafanyakazi ambao umewapa mafanikio hayo kwa kipindi kifupi tangu waingie kwenye sekta hiyo.

'' Niwaombe viongozi wa kampuni hii waendelee kuwa wabunifu kwa kujifunza zaidi kutoka kwa makampuni yenye uzoefu naamini ndani ya miaka miwili ijayo Jostano Trans watakuwa wabobezi wakubwa kwenye sekta hii kwani wameanza vizuri,'' alisema Alex.

Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ] UDSM }, Amina Seif ambaye alisafiri na basi la kampuni hiyo kutoka Singida kwenda Dar es Salaam alisema muda wanaoambiwa kufika Dar es Salaam kutoka Singida unakuwa ni uleule wa saa 11 na nusu jioni tofauti na mabasi mengine ambayo yanafika kuanzia saa 12 jioni hadi saa mbili na kuendelea.

''Abiria waliowengi hawapendi longolongo wanapenda kufika muda uleule walioambiwa labda tu ziwepochangamoto za kuharibika kwa gari lakini za kukamatwa na trafiki zinaweza kuepukika kwa kuzingatia sheria za usalama barabarani kama za mwendo kasi, uchakavu wa gari na matairi,'' alisema Seif.

Alisema lugha nzuri wakati wa utoaji huduma kwa abiria ni jambo lingine ambalo limemfanya avutike na kusafiri kwa kutumia mabasi hayo na utaratibu wa kuomba dua wakati wa kuanza safari na baada ya kufika.

Wakala wa mabasi katika Stendi Kuu ya Mabasi Mkoa wa Singida aliyejitambulisha kwa jina la Awadhi Sendoro  alisema amefanya kazi hiyo kwa muda mrefu katika stendi hiyo na kueleza kuwa kampuni hiyo kwa muda mfupi tangu ianze kufanya kazi imekuwa na wateja wengi.

'' Mimi sio wakala wa mabasi hayo lakini kutokana na watu wengi kuwa na namba zangu wamekuwa wakinipigia simu niwashikie nafasi katika mabasi hayo na nimekuwa nikifanya hivyo,'' alisema Sendoro.

Alisema abiria wengi wamekuwa wakipenda kusafiri na magari hayo kwa sababu ya huduma nzuri wanazozipata na kufika muda wanaoambiwa na mwendo mzuri wa mabasi hayo.

Katibu Mkuu Kiongozi wa Kampuni hiyo hiyo, Elias Meko alisema mafanikio hayo waliyoyapata kwa muda mfupi yanatokana na ushirikiano baaina ya viongozi wa kampuni hiyo pamoja na wafanyakazi ambao wakati wote ndio wanaokuwa na abiria.

'' Tumekuwa tukikutana na wafanyakazi wetu wa kada zote wakiwemo makondakta na madereva na kufanyanao vikao kazi kwa ajili ya kukumbushana majukumu ambayo matunda yake ndiyo mafanikio haya yanayoonekana kwa abiria tunao wahudumia,'' alisema Meko. 

Alisema kampuni hiyo ilianza rasmi kufanya kazi zake mwaka 2021 kati ya Singida na Babati Manyara na baadae Singida, Dodoma, Morogoro na Dar es Salaam.

Meko alisema hivi sasa wameanzisha safari ya kutoka Singida kwenda Mbeya na kuwa kampuni yao hivi sasa imekuwa bora na kimbilio kwa wananchi wanaosafiri kwa mabasi yao.

Alisema licha ya kuwepo na ushindani wa kibiashara hali sio mbaya hasa ukizingatia kuwa hawana muda mrefu tangu waingie kwenye sekta hiyo na amewaomba wananchi kuendelea kuwaamini na kuwaunga mkono zaidi na wao wataendelea kuwapa ushirikiano lengo likiwa ni kuunga mkono jitihada za Serikali chini ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha sekta ya usafirishaji inakua na kutoa huduma bora kwa wananchi.

Katibu Mkuu huyo Kiongozi alisema wamekuwa na safari zao kila siku kutoka Singida kwenda Dares Salaam, Dar es Salaam kwenda Singida, Singida kwenda Mbeya na Mbeya kwenda Singida na kuwa tiketi zao zinapatikana kwa njia ya mtandao www.jostano.co.tz na www.busbora.co.tz.

Alisema namna ya kununua tiketi zao kwa njia ya mtandao hatua ya kwanza ni tembelea www.jostano.co.tz au pakua BUSBORA APP kutoka google play Store busbora.co.tz.

Alitaja hatua ya pili ni kuchagua unapotoka na unapotaka kwenda na tarehe ya safari kisha 'TAFUTA'

Meko alitaja hatua ya tatu kuwa Chagua Bus la Jostano Trans kisha '' ONYESHA SITI''  chagua siti uipendayo, chagua kituo cha kushukia na kupandia. Jaza majina kamili, namba ya simu, jinsi kisha endelea.

Alitaja hatua ya nne ni hakikisha taarifa za safari yako na kisha ENDELEA NA MALIPO.

Alitaja hatua ya tano kuwa ni chagua mtandao wa malipo kisha fuata maelekezo yanayojitokjeza kulipia.

Alitaja hatua ya mwisho kuwa mara baada ya malipo utapokea ujumbe wenye uthibitisho wa tiketi na utaweza kupakua nakala ya tiketi katika kifaa chako.

Meko alisema vitu vya kuzingatia kuwa ni vigezo na masharti vilivyowekwa ni nauli iliyowekwa kwenye tiketi haibadilishwi, kuzingatia muda wa safari na abiria afike kwenye kituo cha kupandia bus kabla ya nusu, mzigo wa ziada utakaozidi kilo 20 utatozwa nauli,  mzigo wa mkononi wa abiria sio dhamana yao, abiria akisitisha safari atoe taarifa saa 12 kabla ya safari na atakatwa asilimia 15 ya nauli aliyolipa.

Alitaja vigezo na masharti mengine kuwa ni iwapo abiria atasitisha safari pasipo kutoa taarifa au kuachwa na basi kwa kuchelewa  kufika kituo cha kupanda nauli haitarudishwa.

Alisema viongozi wa kampuni hiyo wapo tayari wakati wote kupokea maoni mbalimbali wanayoletewa na wasafiri wao na kuyafanyia kazi mara moja ikiwa ni ni moja ya njia ya kuboresha huduma zao.

Alisema kila penye mafanikio hapakosi kuwa na changamoto za hapa na pale hivyo aliwaomba wateja wao kuendelea kuwaamini na kwa changamoto zilizojitokeza wakati wa safari zao wanaomba wawasamehe,

Pia Meko ameendelea kuwahimiza wateja wao kukata tiketi kwenye ofisi zao  au kwa njia ya mtandao jambo litakalosaidia kuondoa changamoto za kuzidishiwa nauli na kutapeliwa,

Katika hatua nyingine Meko amesema kampuni hiyo itakuwa na uchoyo wa fadhira iwapo itashindwa kumshuru na kuthamini mchango wa Kampuni ya mabasi ya Happy Nation katika mchango mkubwa wa ukuaji wa kampuni yao ya Jostano Trans na kuwa wanashirikiana viziri na Mkurugenzi wa kampuni hiyo ndugu Issa ambaye amekuwa hachoki kushiriukiana nao katika kila jambo la kuboresha utendaji kazi ambao umewaletea mafanikio hayo.  

Aidha, alitaja namba za mawakala wao kuwa ni 0683-712030 Makao Makuu Dar es Salaam, 0765-290928 Singida, 0786-292792 na 0759-500010 Dar es Salaam, 0785-776402 Dodoma , 0655-900909 Morogoro na Mbeya ni 0752-397910.

Wafanyakazi wa  Basi namba T 133 DEA wakiwa mbele ya basi hilo tayari kwa safari ya Dar es Salaam kwenda Singida.Kushoto ni Dereva Hamad Athuman na kulia ni Kondakta Martha William.
Abiria wakiingia katika basi Stendi kuu ya mabasi Singida.
Wafanyakazi wa mabasi hayo wakiwa mbele ya moja ya mabasi hayo kabla ya kuanza safari. Kuitoka kushoto ni Kondakta wa mabasi hayo Martha William, Msimamizi wa Usalama na haki za abiria upande wa Dar es Salaam,  Ally Atuman na kulia ni  Ofisa Mwandamizi wa Ofisi ya kampuni hiyo Makao Makuu Dar es Salaam, Vanessa Samwel.
Basi la kampuni hiyo linalofanya safari zake kati ya Mbeya na Singida likiwa safarini. 

No comments:

Post a Comment