Habari za Hivi Punde

6/recent/ticker-posts

Header Ads Widget

FUNDI NGUO ANYAKUA PIKIPIKI PROMOSHENI YA AIRTEL SANTA MIZAWADI

 Mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando akizungumzia kuhusu droo hiyo.

.................................

Na  Phabyola Sumary, Dar es Salaam

MJASIRIAMALI wa kushona nguo Fatuma Mwandege mkazi wa Ukonga Majumba Sita jijini Dar es Salaam amepata zawadi ya pikipiki baada ya kuibuka kidedea katika promosheni inayo endeshwa na Airtel Tanzania ya Santa Mizawadi.

Mwandege amepata zawadi hiyo pamoja na wenzake ambao wameshinda zawadi mbalimbali zikiwemo runinga, simu janja, pocket WiFi, fedha taslim Sh.Milioni 1 na nyingine nyingi.

Mwandege ameishukuru kampuni hiyo ya simu kwa kuendesha promosheni hiyo kwa ajili ya wateja wake na mawakala ambao wanakwenda kuongeza kasi ya kutumia huduma mbalimbali za Airtel.

Mwanamke huyo na wenzake wamejinyakulia zawadi hizo katika droo ya kwanza ya promosheni hiyo ambayo iliyofanyika jana  jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali.

Wengine waliojishindia zawadi mbalimbali ni pamoja na Andrew Chiomo mwendesha bodaboda mkazi wa Ifakara mkoani Morogoro aliyepata fedha taslimu Sh. Milioni 1, Josephine Mgalu mkazi wa Nzega ambaye alijishindia pocket Wifi.

Aidha, washindi wengine ni Omari Ramadhani mkazi wa Shinyanga ambaye amepata simu aina ya smart phone na Halima Kimaro ambaye naye ni mkazi wa Shinyanga ambaye alijishindia Runinga inchi 55 na washindi wengine ambao walijinyakulia zawadi za aina tofauti tofauti.

Akizugumza wakati wa promosheni hiyo Mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano wa kampuni hiyo, Jackson Mmbando  alisema  promesheni hiyo  inaendelea hadi mwezi Januari mwakani na kuwa itakuwa ikifanyika kila wiki.

Amesema Airtel Santa Mizawadi ni promosheni ambayo imelenga kutoa shukurani kwa wateja wao na mawakala ambao wanaendelea kutumia huduma za kampuni hiyo.

Mmbando alitaja zawadi zinazotolewa kwa washindi hao kuwa ni pocket WiFi, simu janja, pikipiki, runinga na pesa Taslim Shilingi milioni moja.

Alisema jinsi ya kushiriki na  kujishindia mizawadi hiyo wateja wao na mawakala wanatakiwa kufanya miamala ya kuweka na kutoa fedha, ambapo pia ili Mteja aweze kuingia kwenye droo anatakiwa kufanya miamala ya kununua bando, Kutuma pesa,  kutoa pesa, kulipa bili, kufanya miamala ya kibenki, kutuma au kupokea pesa nje ya nchi na kununua  muda wa maongezi.

Droo hiyo ikiendelea.
 

Post a Comment

0 Comments