JESHI LA POLISI KUENDELEA KUTUMIA MIFUMO YA KIELEKTRONIKI ILI KUDHIBITI MATUMIZI YA FEDHA ZA UMMA. - MTAZAMO MEDIA

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Saturday, 15 March 2025

demo-image

JESHI LA POLISI KUENDELEA KUTUMIA MIFUMO YA KIELEKTRONIKI ILI KUDHIBITI MATUMIZI YA FEDHA ZA UMMA.

Responsive Ads Here

CrcmP1xWIAIjnXD

Jeshi la Polisi nchini limesema linaendelea na mikakati ya kutumia mifumo mbalimbali ya kielektroniki iliyoanzishwa na serikali, ambayo itasadia kuleta uwazi, uwajibikaji na udhibiti wa matumizi ya fedha za umma.

Hayo yamesemwa na Kamishna wa Fedha na Lojistiki wa Jeshi la Polisi, CP Liberati Sabas wakati akifungua kikao kazi cha Maafisa Wanadhimu na Wahasibu wa Jeshi la Polisi kutoka Makao Makuu, Mikoa, Vikosi na Vyuo, katika shule ya Polisi Tanzania (TPS - Moshi ) mkoani Kilimanjari Machi 14, 2025.

CP Sabas amewataka Maafisa wanadhimu na Wahasibu kwenda kuwajibika ipasavyo katika maeneo yao ikiwa ni pamoja na kuwasimamia watendaji wa chini yao kutumia vyema mifumo hiyo sambamba na kusimamia fedha zote ambazo ziliainishwa na serikali kwa mwaka wa fedha 2024/ 2025 kwa kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma.

Kikao kazi cha Maafisa Wanadhimu na Wahasibu wa Jeshi la Polisi kutoka Makao Makuu, Mikoa, Vikosi na Vyuo hufanyika kila mwaka kwa lengo la kujadili mambo mbalimbali yanayohusu masuala ya usimamizi wa rasilimali fedha ndani ya Jeshi la Polisi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Pages

Contact Form

Name

Email *

Message *