Random Posts

DR.MVUNGI AFARIKI DUNIA LEO, MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI

RAISKIKWETE 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma Kikwete na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi Mhe. James Mbatia na daktari wa zamu wakimwangalia Mjumbe wa Tume ya Katiba Dkt. Sengondo Mvungi alipokuwa amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha Mifupa (MOI)  Oktoba 3, 2013 kufuatia kujeruhiwa kwake na watu wanaosadikiwa ni majambazi usiku wa Jumamosi Oktoba 2, 2013.

(PICHA NA IKULU)

TAARIFA ZILIZOTUFIKIA KITENGO CHA HABARI KATIKA MTANDAO WAKO WA www.fullshangweblog.com ZINASEMA KUWA MJUMBE WA TUME YA KATIBA ALIYEJERUHIWA NA WATU WANAOSADIKIKA NI MAJAMBAZI USIKU WA JUMAMOSI OKTOBA 2 MWAKA HUU, DKT. SENGONDO MVUNGI , AMEFARIKI DUNIA LEO ALASIRI NCHINI AFRIKA KUSINI ALIPOKUWA AKITIBIWA.
MWENYEKITI WA CHAMA CHA NCCR-MAGEUZI NA MBUNGE WA KUTEULIWA MHE. JAMES MBATIA AMETHIBITISHA KUTOKEA KWA KIFO HICHO CHA DKT. MVUNGI ALIYEWAHI KUWA KIONGOZI MKUBWA WA CHAMA HICHO.
KITENGO CHA HABARI KINAFUATILIA KWA KINA TAARIFA HIZO, TAFADHALI ENDELEA KUWA NASI.
CREW NZIMA YA MTANDAO HUU INATOA POLE KWA WATANZANIA WOTE WAKATI HUU WA MAJONZI.
MWENYEZI MUNGU AWAPE NGUVU.
AMINA

Post a Comment

0 Comments