................
Wamachinga yaani wale wafanya biashara ndogondogo wasio na sehemu maalumu ya kufanyia
biashara,na Bodaboda`inaonekana wamepuuza amri ya Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam
na halimashauli za jiji ya kuwapiga marufuku
kufanya biashara sehemu ,ambazo sio rasmi na kwenda katika
maeneo yaliyotengwa maalum kwa ajili ya
biashara zao.hii imejidhihilisha hivi leo maeneo ya kariakoo,wamachinga
wamerudi tena nakufanya mitaa ya kongo kuwa napurukushani.pamoja na wamachinga
kurudi kinyemela kariakoo,nao askari wa jiji wamewafanya machinga kama ndio
mradi wao wa kujiingzia pesa haram ,wamekuwa wana wakamata nakuwaomba pesa
kuanzia elfu 10 ,hivyo kufanya zoezi lilliotangazwa na mkuu wa mkoa .kuwa gumu
wakati lilikuwa ni rahisi.
Hali ya rushwa nchini imekuwa ni donda ndugu.pamoja na Mhe
Rais kulivalia njuga kulikomesha ,Tatizo ni wale waliokabiziwa jukumu la
kulishugulikia
Nao polisi wa barabarani na ulinzi shilikishi wamefanya
bodaboda mradi,
Bodaboda wameamua makusudi kuvuruga utaratibu waliowekewa
wakuto kuingia katikati ya jiji kinyume kabisa tena kwa jeuri ,wanaingia katika
ya jiji nakusababisha ajari nyingi,na hawafati utaratibu imekuwa ni fujo na
kero .Polisi wa barabarani wanawakamata na kuwaachia katika mazingila ya kutatanisha,bado
kuna haja ya serikali kuwaangalia kwa
jicho la umakini bodaboda kwa kuwachukulia hatua kali zaidi ,hakuna kitu
kinachoshindikana mbona Waziri wa uchukuzi Mhe Dk Mwakyembe ameweza
kumaliza,kero zilizo kuwa zinatokea bandarini?aliuliza Jumanne Hasani mkazi wa
ilala.