Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha
Kusambaza Matrekta kwa Wakulima ya Kariati Matractor , Omary Kariati
(kulia), akimkaribisha mgeni rasmi Mke wa Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikianmo wa Kimataifa, Mama Dorcas Membe wakati akiwasili katika
hafla ya kufungua kituo hicho kilichopo Kinondoni Dar es Salaam leo
asubuhi.
PICHA ZOTE NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE
.............................................
Mke wa Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikianmo wa Kimataifa, Mama Dorcas Membe (katikati), akisalimiana na
Meneja wa Uhusiano kwa Wateja Wakubwa wa Benki ya KCB, Victor Malewo,
ambapo wamekiwezesha kituo hicho kupata mikopo ya kununulia matrekta
hao.
Mke wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikianmo wa Kimataifa, Mama Dorcas Membe na Mkurugenzi
Mtendaji wa Kituo cha Kusambaza Matrekta kwa Wakulima ya Kariati
Matractor , Omary Kariati wakionesha tovuti ya kituo hicho baada ya
kufungulia. Tovuti hiyo ya www.kariatimatractor.com itamsaidia mkulima
yeyote aliopo nchini kupata fomu kwa ajili ya kununua matrekta hayo.
Mke wa Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikianmo wa Kimataifa, Mama Dorcas Membe (katikati), akikata utepe
kuashiria ufunguzi wa Kituo cha Kusambaza Matrekta cha Kariati Matractor
kilichopo Kinondoni Dar es Salaam jana. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo hicho, Omary Kariati na Meneja wa Uhusiano kwa Wateja Wakubwa wa Benki ya KCB,
Victor Malewo, ambapo wamekiwezesha kituo hicho kupata mikopo ya
kununulia matrekta hayo.















