Watuhumiwa wa ujangili
ambao ni Mtendaji wa Kijiji (kushoto) na mwenzake wakiwa wameshika nyara za
Serikali walizokamatwa nazo huko Mbwewe, wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani.
...............................................................................................................................................
WAWILI WAKAMATWA NA NYARA
ZA SERIKALI NGOZI YA CHUI YA THAMANI YA SH. MILIONI 10
Na
Bernard james wa Mtazamomedia
Jeshi
la polisi mkoa wa Katavai kwa kushirikiana na askari wa hifadhi ya Taifa ya
Katavi wamewakata watu wawili wakiwa na nyara za serikali ngozi ya chui mbili
zenye thamanai ya zaidi ya milioni 10.
Kaimu
kamanda wa polisi wa mkoa wa Katavi kamishina msaidizi Emmanuel Nlay aliwataja
waliokamatwa ni Komanya Luponya (28) mkazi wa kijiji cha Mbede wilaya ya Mlelel
na Heleni Jilala (20) mkazi wa Muzye Sumbawanga mkoani Rukwa
Alisema
watuhumiwa hao walikamatwa Mei 22 mwaka huu majira ya saa moja asubuhi katika
eneo la kijiji cha Mwamadulu tarafa ya Mpimbwe wilaya ya Mlele mkoa wa katavi.
Watuhumiwa
hao walikamatwa kufuatia taaraifa zilizokuwa zimelifikia jeshi la polisi kuwa
watu hao wanajihusisha na uwindaji haramu katika hifadhi ya taifa ya katavi.
Nlay
alieleza polisi kwa kushirikiana na askari wa ifadhi ya katavi
walifanikiwa kuwakuta watuhumiwa wakiwa kwenye kambi waliyofikia ambayo
ilikuwa ni kwa ajili ya malisho ya ng’ombe.
Baada
ya kupkuliwa watuhumiwa walikutwa na nyara za serikali ngozi mbili za chui
zenye thamani ya shilingi Tsh. 10,500,000/=
Kaimu
kamanda Nlay alieleza watuhumiwa watafikishwa mahakamani mara baada ya
uchunguzi kuwa umekamilika ili waweze kujibu mashitaka ya kukamatwa na
nyara za serikali
Wakati
wa kongamano la kimataifa lililo kutanisha wadau mbalimbali kutoka nchi
mbalimbali Duniani.Waziri wa Maliasili Mhe Lazaro Nyalandu alisema amejipanga
kuakikisha ujangiri hapa nchini anautokomeza kwa mbinu ya aina yoyote ile.na
tatizo la ujangiri linamkera sana.Nyalandu alisema tayari Wizara imeisha unda
kikosi kazi na vijana tayari wapo site ,Wizara tayari imeisha pata silaha za kisasa
kukabiliana na majangili ambao wanatumia silaha kali za kivita alisema Nyalandu .kukamatwa kwa wafugaji wakiwa na ngozi za
chui nikielelezo tosha kwamba wafugaji wanatumiwa na majangili.Serikali imekuwa
inawakataza wafugaji kuingiza mifugo yao ndani ya hifadhi ya Taifa kulisha
mifugo .
