Msanii Snura Mushi (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imeruhusu kupigwa kwa wimbo wa chura ya kuufunga kwa kuwa haukuwa na maudhui mazuri ya kitanzania. Kushoto ni Msemaji wake, Baraka Nyagenda.
............................................................................................
Msanii wa bongo flaver
snura mushi akubaliwa kuendelea kutumia wimbo wake wachura uliokuja na video
mpya ukiachana na video ya awali iliyokuwa haina maadili ya kitanzania wimbo
huu awali ulitangazwa kufungiwa tarehe 3/5/2016 na tarehe 5/5/2016 msanii huyu
aliomba radhi kwa serikali na umma kwa ujumla.
Akizungumza na
waandishi wa habari katika ukumbi wa Maisha Bezmet-makumbusholeo amesema kuwa kwanza kabisa anamshukuru waziri
Nape Nauye kwa kuruhusu wimbo wa chura ulioambatana na video mpya kurushwa, na
kuonyeshwa katika vituo vya TV na Radio baada ya kuona wimbo huu kwa sasa
umekuja na video yenye maadili ya kitanzania na sikupotosha maadili kama
zamani.
“namsukuru mheshimiwa
waziri Nape Nauye kwa kuruusu wimbowangu wa chura uliombatana na video mpya
yenye maadili kurushwa katika televition na radio kama tulivyokuwa
tumekubaliana awali kwamba wimbo wangu mpyua utafunguliwa endapo nitakuja na
video mpya yenye maadili”
Kutokana na watu wengi
kutoelewa maana halisi ya wimbo huo msanii huyo ameeleza nini ilikuwa maana na
lengo la wimbo huo kwasababu awali watu wali imba wimbo na kutoa maana zao
ambazo zilikuwa tofauti na matakwa yake hadi kupelekea wimbo uo kufungwa
“video yangu mpya ya
chura unaeleza maana halisi ya neno chura niliyekuwa namzungumzia ikiwa na maana
kwamba chura anaasili ya kurukaruka na huu wimbo na video imemfananisha chura
na mwanamke asietulia katika mapenzi na kurukaruka na wanaume wengine
linapotokea tatizo la mahusiana na kusababisha magonwa sugu na hii ndio maana
halisi tofauti na watu walivyokuwa wakitafsiri”.
Pamoja na hayo ametoa
shukrani zake kwa wizara ya habari , utamaduni,
sanaa na michezo, kwa elimu aliyopewa ambayo imempa mafunzo na kuahidi
kutorudia kutoa wimbo na video isiyo kuwa na maadili .na mpaka kufikia sasa wimbo wake wa chura
ulioambatana na video mpya upo huru kurushwa ndani na ne ya nchi.
0 Comments