Random Posts

KOCHA PLUIJM AWEKA WAZI SILAHA ZAKE DHIDI YA RUVU SHOOTING LEO,AWATUPA BENCHI KASEKE NA DIDA.

Kocha Mkuu wa Mabingwa watetezi Yanga Hans Van Der Pluim.

..................................................................................

Na.Alex Mathias,Dar es salaam.

Kocha Mkuu wa Mabingwa watetezi Yanga Hans Van Der Pluim,kuelekea mchezo wake dhidi ya Ruvu Shooting majira ya saa kumi jioni ametangaza kikosi kitakachoanza huku akiendelea kuwachunia walinda mlango wake na kumuamini Kakolanya.

Mchezo huu unatarajiwa kuchezwa katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam huku wana jangwani hao wataingia na hasira na morali baada ya watani zao Simba kufungwa jana na Prisons hivyo endapo watashinda watakuwa wamebakiza pigo la pointi mbili hata wakifungwa watabaki nafasi hiyo hiyo ya pili.

Kikosi cha Leo ni:Beno Kakolanya,Hassani Kessy,Mwinyi Haji,Kelvin Yondani,Vicent Andrew,Thabani Kamusoko,Haruna Niyonzima,Amis Tambwe,Donaldo Ngoma na Obrey Chirwa.

Wachezaji wa Akiba:Deogratius Munish,Oscar Joshua,Pato Ngonyani,Deus Kaseke,Anthony Mateo,Said Makapu na Juma Mahadhi.

Baada ya kumalizika kwa mchezo huo Ligi itasimama na kusubiri raundi ya pili ya mzunguko wa Vodacom Tanzania bara na kuanzia Novemba 15 timu zote zitaanza usajili rasmi uliotangazwa na Shirikisho la mpira wa Miguu Tanzania.

Post a Comment

0 Comments