Random Posts

YANGA YANG'ARA LIGI KUU TANZANIA YAICHAPA RUVU SHOOTING,PLUIJM AONDOKA KWA HUZUNI.

Na.Alex Mathias,Dar es salaam.

Mabingwa watetezi Yanga wamemaliza duru ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania bara kwa ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Ruvu Shooting mchezo uliochezwa katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Abrahman Mussa alikuwa wa kwanza kuifungia Ruvu dakika ya 7 baada ya kuwazidi ujanja walinzi wa Yanga chini ya Dante na Yondani licha ya kutanguliwa goli hilo Yanga waliendelea kulishambulia lango wa Ruvu huku wageni wakicheza mchezo wa kujilinda  zaidi.

Haruna Niyonzima alitoa pasi ya goli kwa Simon Msuva katika dakika ya 31 na kuisawazishia Yanga baada ya kupata goli hilo Ruvu waliendelea kucheza kwa kujilinda na kuruhusu mashambulizi mengi huku washambuliaji Msuva,Ngoma,Chirwa na Tambwe wakishindwa kutumia nafasi vizuri hadi mapumziko timu hizo zilienda nguvu sawa.

Kipindi cha pili kilianza kwa Yanga kupata pigo baada ya kocha wao Mkuu Hans Van Der Pluijm,alitolewa nje ya uwanja kwa kuoneshwa kadi kutokana na kutoa lawama nyingi kwa wamuzi wa mchezo huo licha ya kupata pigo mabingwa hao waliendelea kutafuta pointi tatu muhimu.

Haruna Niyonzima ambaye ndio alikuwa nyota wa mchezo aliifungia goli la pili na la ushindi dakika ya 56 kwa shuti kali akipokea pasi ya Ngoma baada ya kumtoka golikipa wa Ruvu hadi mwamuzi Mathew Akhrama toka Mwanza anapuliza kipyenga cha mwisho Yanga wameibuka na ushindi wa magoli 2-1.

Kwa matokeo hayo Yanga wamefikisha pointi 33 na kuwa nyuma ya Simba wa pointi mbili wanaongoza Ligi wakiwa na Pointi 35 na Ligi hiyo itasimama na kuanza duru la pili mwakani Januari na huu mchezo kwa tetezi za chini ulikuwa wa mwisho kwa Kocha Hans Van Der Pluijm ambaye atampisha Mzambia Goerge Lwandamina.

Post a Comment

0 Comments