Random Posts

WAZIRI NAPE AMKABIDHI TUZO YA HESHIMA DJ BONY LOVE KATIKA TUZO ZA EATV AWARDSZILIZOFANYIKA USIKU HUU KWENYE UKUMBI WA MLIMANI CITY JIJINI DAR ES SALAAM

1
Waziri wa Habari, Utamaduni ,Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye akikabidhi Tuzo ya Heshima kwa DJ Boniventura Kilosa aka Bony Love baada ya kutangazwa mshindi wa heshima katika tuzo za EATV AWARDS 2016 zilizofanyika  usiku huu  kwenye ukumbi wa Malimani City jijini Dar es salaam.

Tuzo hizo zinaandaliwa na kituo cha Televisheni cha EATV cha jijini Dar es salaam kinachorusha matangazo yake katika nchi za Afrika Mashariki.
5
Mwanamuziki Lady Jay Dee akipongezwa na Mpenzi wake Rama D. mara baada ya kupokea tuzo yake  katika hafla ya utoaji wa tuzo za  EATV AWARDS zilizofanyika kwenye ukumbi wa Malimani City jijini Dar es salaam.
4
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye akimsikiliza DJ Boniventura Kilosa aka Bony Love alipokuwa akitoa shukurani zake mara baada ya kupokea tuzo yake ya heshima iliyotolewa na EATV.
3
DJ Boniventura Kilosa aka Bony Love akizungumza machache huku rafiki yake John Dilinga akiwa ameshika tuzo hiyo.
2
DJ Boniventura Kilosa aka Bony Love akipongezwa na DJ John Dilinga mara baada ya kupokea tuzo yake ya Heshima katika tuzo zilizoandaliwa na Kituo cha Televisheni cha EATV.
6
Mwanamuziki Lady Jay Dee akitumbuiza katika tuzo hizo.
5
Mshindi wa filamu bora ya mwaka anayejulikana kwa jina la Gabo akizungumza mara baada ya kupokea tuzo yake usiku huu kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
2
Mwanamuziki Ali Kiba akizungumza mara baada ya kupokea tuzo yake.
1
Mwanamuziki Ali Kiba akipokea tuzo yake ya ushindiwa Wimbo Bora wa Mwaka kutoka kwa Nandi Mwiyombela kutoka kampuni ya Vodaco Tanzania katika Tuzo za Muziki za EATV AWARDS zinazofanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.


3
Add caption
4 3 16 15 14 13 12 11 10 8 7 6 5 4 1

Post a Comment

0 Comments