Random Posts

MKUU WA MKOA WA MBEYA AZITAKA HALMASHAURI ZOTE MKOA WA MBEYA KUPATA HATI SAFI

 Hati chafu ni Matokeo YA kutozingatia taratibu za Fedha  WANANCHI wanapunguza imani kwa halmashauri zao kupata hati za mashaka 
 Azikumbusha halmashauri kutenga asilimia 10 YA mapato YA ndani kwa ajili YA mikopo YA wanawake na vijana  Mkuu wa Mkoa wa Mbeya leo amekutana na wakuu wa wilaya, wakurugenzi, wakuu wa idara wa halmashauri zote katika kikao cha  kawaida cha  kupokea na kupitia taarifa za kudhibiti mapato na matumizi za halmashauri  na kuzitaka halmashauri hizo kufuata taratibu za Fedha katika shughuli za kila siku na kufanya hivyo wataepuka kupata hati chafu
Amesema halmashauri inapopata hati chafu wananchi hupunguza imani kwa halmashauri yao hivyo ni vema jitihada za makusudi zifanywe  ikiwemo kuzingatia ushauri wa CAG, mkaguzi wa ndani na kufuata taratibu za Fedha kutasaidia kupata hati safi

Post a Comment

0 Comments