MVUA YASABABISHA KAYA 20 CHALINZE MZEE KUKOSA PAKUISHI - MTAZAMO MEDIA

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Saturday, 8 April 2017

MVUA YASABABISHA KAYA 20 CHALINZE MZEE KUKOSA PAKUISHI

Nyumba mbalimbali zikionekana kubomoka na kuezuliwa mapaa na mvua iliyoambatana na upepo ambayo imenyesha huko Chalinze Mzee ,jimbo la Chalinze mkoani Pwani. Kufuatia maafa hayo, mbunge wa jimbo hilo Ridhiwani Kikwete amewatembelea waathirika waliokumbwa na adha hiyo.

 (Picha na Mwamvua Mwinyi) 
.........

     Na Mwamvua Mwinyi   

   MVUA inayoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali mkoani Pwani hususan,  jimbo la Chalinze  imeleta madhara huko eneo la Chalinze Mzee ambapo kaya zaidi ya 20 zimekosa makazi ya kuishi. 

 Aidha nyumba tisa zimesombwa na maji na nyingine kubomoka hali inayosababisha wakazi wa nyumba hizo kuishi kwa kusaidiwa na ndugu na majamaa. 

Kutokana na hali hiyo, mbunge wa Jimbo la Chalinze ,Ridhiwani Kikwete,ametembelea eneo la Chalinze Mzee lilokumbwa na mafuriko kutokana na mvua hizo. 
 Ridhiwani alitoa pole kwa waathirika waliokumbwa na maafa hayo .

Alitaja  maeneo yaliyokumbwa na  mafuriko ni Chalinze Mzee,Bwawa la umwangiliaji la Msoga ambalo limetoboka na shule ya Sekondari ya Imperial.

Aidha,Ridhiwani alieleza kuwa madhara makubwa yaliyotokana na mafuriko hayo ni kuharibika kwa mashamba,nyumba za wananchi kuharibika na  wananchi kukosa pakuishi.

Mbunge huyo aliongeza kwamba  kwasasa wananchi hao wanahitaji msaada hivyo aliwaomba wadau wa maendeleo ya jamii kuwasaidia kwa hali na mali.

         "Ni maafa makubwa inabidi yatuguse wote  niwaombe wadau wengine washirikiane na serikali na mi mbunge kuwawezesha yale yaliyokwenye uwezo wetu watu hawa "alisema Ridhiwani. 


Kwa upande wao baadhi ya wakazi waliokumbwa na kadhia hiyo walisema mvua iliyoambatana na upepo mkali ,imeezua mapaa ya nyumba na nyingine kubomoka na kusababisha familia za nyumba hizo kuhaha kukosa pakuishi. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages