Subscribe Us

header ads

ZAIDI YA WATU 70 WAOKOLEWA LEO KUTOKANA NA MAFURIKO YALIYOTOKANA NA MVUA KUBWA

Mkazi wa Omukigusha akisaidiwa kuvutwa juu baada ya kuanguka shimoni asubuhi leo kwenye mufda wa saa nne.

 Picha na habari na Faustine Ruta
.........
 Faustine Ruta, Bukoba

 ZAIDI ya watu 70 wameokolewa na Serikali baada ya kukumbwa na mafuliko yaliyotokana na mvua iliyoanza kunyesha kuanzia saa 9 usiku. 
Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa wilaya ya Bukoba Deodatus Kinawilo wakati alipo hojiwa na waandishi wa habari katika Kata ya Bakoba mtaa wa nyakanyasi. 
Kinawilo alisema kuwa nyumba zote zilizoko kandokando ya mto kanoni zote zimeathiliwa na maji kiasi kwamba tumetumia mitumbwi ya uvuvi kuvusha watu. 
“Niseme tu mpaka sasa hakuna kifo chochote kile Zaidi ya vitu kuhalibika kwa kulowa maji”alisema kinawilo 

Aidha mkuu wawilaya alisema kuwa kuwa wananchi wachukue tahadhali pindi mvua zinapo nyesha tu watoke nje ya nyumba kwa usalama Zaidi. 

Naye Josefati Bonge mkazi wa Omukigusha alisema kuwa katika nyumba yake hakuna kilichobakia kikiwa kizima kwani nimetoka mimi kama nilivyo na ninamshukuru mungu familia yangu haikuwepo. 

“Kiukweli kuna kila sababu ya kuhama maeneo kama haya maana nihatali kwa binadamu mfano’ waliokuwa wamelala fofo wanahali gani hivyo kunatakiwa kuchua hatua mapema ili kuhamia sehemu stahiki”alisema Bonge 
Anitha Mziba mkazi wa Nyakanyasi alisema kuwa yeye katika familia yake hakuna alie umia Zaidi ya vitu vyote vyandani hakuna kilichotoka.

“Yani nimewabeba watoto wangu begani mmoja baada ya mwingine wakati huo mimi maji yakiwa yamenifikia kwenye shingo kwakweli nihatali”alisema Mziba
 Katikati ya Makazi ya watu Eneo la Nyakanyasi Mitumbwi imefanya kazi
 Okoa okoa ikiendelea eneo la Nyakanyasi Mjini Bukoba leo hii
 Wakaazi wa hapa Tangu usiku saa 9 waliondoka!
 Eneo la Ziwa Victoria...Ufukweni
 Prince Motel
 Crane Lodge and Tours
 Hii ni nyumba ya Wageni...lakini inasemekana Usiku hawakupata usingizi kabisa!
 Patashika wakazi wakiokoa Nyasi kwa ajili ya Mifugo yao
 Mkazi wa Nyakanyasi akivuka huku akiwa hana matumaini Aendako

Post a Comment

0 Comments