Random Posts

Tume ya Taifa ya Uchaguzi Yaitahadharisha Cuf

Na Margareth Chambiri, NEC
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imekishauri Chama cha Wananchi (CUF) kumalizamgogorounaoendelea ndani ya Chama hicho kwani unawezakusababishakupotezanafasi za Udiwani katika Uchaguzi Mdogounaotarajiwakufanyikawakatowowote kuanzia sasa.

Tahadhari hiyo imetolewaleo na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume hiyo Bw. Kailima Ramadhani katika 

mahojianomaalumOfisinikwakekuhusutuhumambalimbalizilizoelekezwa Tume hiyo ikiwemosuala la Uteuzi wa Wabunge wa VitiMaalumkupitia CUF.

Bw. Kailima amesemamvutanounaoendelea ndani ya Chama cha Wananchi (CUF) haunatija, hivyo ameshauripande mbili zinazovutanakukutananakumalizatofauti zao kwani hali hiyo itawanyimanafasi ya kutoa wagombea kwenye uchaguzihuomdogo.
‘Mimi niwashauri,CUF wanamgogoro wao wamalizemgogoro wao. 

Ni vizuriwakutanewamalizemgogoro wao kwani hii inawezakuwaleteamatatizowagombea wakati wa Uchaguzi.’ alisesemaKailima na kusisitiza kuwa mgogoro ndani ya chamahichohaunatija na badalayakeunakidhoofisha.

AmesemaSheria ya Taifa ya Uchaguzi, inakitakaChama cha SiasakumsimamishaMgombeammoja kwa nafasi moja, lakinipiamgombea wa nafasi ya Rais na Mbungelazimafomuyakeisainiwe na Viongozi wa ngazi ya Taifa wanaotambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa.

‘LakiniukisomaMaelekezo ya Vyama vya SiasanaWagombeayanasemaiwapochama cha Siasakina mgogoroni lazimafomu zakezisainiwa na kiongozi wajuu wa ngazi ya Mkoa, sasa kwa hali hii iwapo CUF wasipokutanawatapotezanafasi.’ Amesema Mkurugenzi huyowa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Bwana Kailimaamesema Tume ya Taifa ya Uchaguzi inatambua taarifa za Vyama vya SiasailiyowasilishwanaMsajili wa Vyama vya Siasa na kwa Chama cha CUF viongozi wanaotambuliwa na Tume hadi hivisasa ni Mwenyekiti Prof. Ibrahim Lipumba na KatibuMkuu ni MaalimSeif Sharif Hamad.

‘Tumeinatambua kuwa Mwenyekiti wa CU ni Prof. Ibrahim Lipumba, InatambuaKatibuMkuu wa CUF ni MaalimSeif Sharif Hamad na NaibuKatibuMkuuupande wa Bara ni Magdalena Sakaya’ amesema.

Amesema TumehaijazuiliwanaMahakamawala na Msajili wa Vyama vya Siasakwambaisifanyemawasiliano na Viongozi hawa, na kubainisha kuwa Tume itaendelea kufanya mawasiliano na Viongozi mpakahapoitakavyoelekezwavinginevyo na Msajili wa Vyama au Mahakama.

Mkurugenzi huyo wa Uchaguzi amesema Tume inafanya kazi kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu na kwambamawasiliano ya Tume na Chama cha Siasa ni kwa mujibu wa maelekezo ya Msajili wa Vyama vya SiasaambayendiyeanayesajiliVyama vya Siasanchini.

Aidha katika hatua nyingine Bwana Kailima ameelezwakusikitishwana taarifa za upotoshajizinazoihusisha Tume kwenye kikao cha Wanasheria kwa lengo la kumshauriSpika wa Bunge kuhusu Chama cha Wananchi CUF na kubainisha kuwa taarifa hizo hazinaukweliwowote.

Akielezea hatua zinazowezakuchukuliwana Tume dhidi ya upotoshwajiunaofanywa na baadhi ya Wanasiasa na Vyombo vya Habari kuhusuutendaji kazi wa Tume Kailima amesema Tume itatumiaMamlakazinazohusika na usajiliingawahata hivyo amesisitiza kuwa ni vyema Vyama vya SiasavitumieWanasheria wao kusomaSheria na taratibu za Uchaguzi ili kupata habari sahihi.


‘Hatua ya kwanza tunayochukua ni hii ya kuelimishaChama pengine ni bahatimbayalakini hatua ya pili ni ya kuzitaarifumamlakaKwa upande wa Vyama ni Msajili wa Vyama kwa upande wa Vyombo vya Habari vya MagazetitunamtaarifuMsajili wa Magazeti ili ashughulikenao’lakinikubwatunawashaurijamanisomeni au ulizeni Tume,’ amesema Kailima. 

Post a Comment

0 Comments