Diwani wa Kata ya Mwaweja, Makanasa
Kishiwa akifungua pazia kuweka jiwe la msingi ujenzi wa moja ya visima saba
vilivyojengwa, hafla iliyofanyika kijiji cha Mwajiginya kata ya Mwaweja.
Diwani wa Kata ya Mwaweja, Makanasa
Kishiwa akizungumza na wananchi katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi.
Mhandisi wa Maji wilaya ya Kishapu,
Lucas Said akizungumza na wananchi katika hafla hiyo.
Mhandisi wa Maji wilaya ya Kishapu, Lucas
Said akitoa maelezo kuhusu namna nyenzo ya kunawia mikono kwa mtu aliyetoa
kujisadia inavyofanya kazi na kumuepusha na maradhi.
Diwani wa Kata ya Mwaweja, Makanasa
Kishiwa akinawa maji safi wakati alipooneshwa nyenzo maalumu kwa ajili ya
kunawa mikono.
Mratibu wa TCRS Kishapu, Oscar Lutenge
akizungumza wakati wa hafla hiyo.
Ofisa Kilimo kata ya Ngofila, Genes
Tarimo akitoa maelezo kuhusu teknolojia rahisi ya kuchemsha maji bila kutumia
nishati ya kuni au mkaa ambayo hsaidia kuhifadhi mazingira.
Kikundi cha kwaya kutoka kata ya
Mwaweja kikitoa burudani iliyoambatana na ujumbe wa kuhifadhi mazingira.
Wananchi wakifuatilia matukio
mbalimbali wakati wa hafla hiyo.
Mafundi wakiwa katika hatua ya mwisho
ya ujenzi wa mojawapo ya visima hivyo.
Wananchi wakifuatilia matukio
mbalimbali katika hafla hiyo.
.............
Na
Robert Hokororo
Wananchi
wa vijiji vya Mwajiginya A, Ubata na Mwaweja wilayani Kishapu mkoani Shinyanga wanatarajia
kunufaika na mradi wa visima vya maji saba mwaka huu.
Hii
ni baada ya kuwekwa jiwe la msingi ujenzi wa visima hivyo vyenye thamani ya sh.
milioni 61.9 uliofadhiliwa na Shirika la Norwegian Church Aid-Tanzania (NCA) likishirikiana
na TCRS pamoja na halmashauri ya Kishapu huku sh. milioni 1.6 zikiwa ni ndugu
za wananchi.
Akizundua
mradi huo, Diwani wa Kata ya Mwaweja, Makanasa Kishiwa alishukuru mashirika
hayo kwa kuchangia shughuli za maendeleo na kuwataka wananchi waibue miradi ya
maendeleo ili Serikali iwachangie.
Alisema
wananchi wana jukumu la kuibua na kuanzisha miradi ili na Serikali kwa
kushirikiana na wadau wa maendeleo iwaunge mkono kwa kutekeleza miradi hiyo.
“Ninyi
wananchi muibue miradi na Serikali itapeleka fedha kuikamilisha, haiwezi kutoa
fedha kwa sehemu ambayo haina mradi hivyo nawaomba mchangamkie fursa hiyo,”
alisema diwani.
Kishiwa
aliongeza kwa kusisitiza kuwa sheria ziwabane wananchi wasiokuwa waaminifu
wanaotumia muda wao kufanya uharibifu wa mazingira katika maeneo mbalimbali.
Ofisa
miradi wa NCA, Zachayo Makobero alisema visima hivyo vitahudumia wananchi 2100
watakaopata maji ndani ya mita 400 kama sera ya maji inavyosema huku 9200
watapata huduma hiyo nje ya umbali wa mita hizo.
Alisema
elimu ya utunzaji wa vyanzo vya maji na usafi wa mazingira kwa kata hiyo na
zingine wilayani humo na vijiji vyake imeendela kutolewa ikiwa ni mwendelezo wa
kampeni zilizofanyika mwaka jana.
Kwa upande wake, Mhandisi wa maji wilaya ya Kishapu, Lucas Said aliwataka wananchi kutunza vyanzo vya maji na kupanda miti ili kuepuka visikauke na kusababisha ukame.
Pia aliwataka kutunza miundombinu ya maji kwani imejengwa kwa gharama kubwa ili kuwahudumia huku akiizitaka kamati za maji vijijini kufanya kazi yake ipasavyo katika kuhudumia wananchi.
Mhandisi Said aliipongeza TCRS kwa kazi nzuri ya kuelimisha na kuhamasisha wananchi utunzaji mazingira na kuwataka wajenge na kutumia vyoo ili kuepuka maradhi.











0 Comments