Naibu
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Ackson akizungumza
na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam Januari 26, 2018 wakati wa hafla ya kupokea
Msaada wa Vifaa kwa ajili ya shule ya Walemavu ya Katumba iliyopo Mkoani Mbeya
Wilaya ya Rungwe (kulia) Mkurugenzi wa Human Relief Foundation Sheikh
Khalid Butchery.
..............
NAIBU Spika Tulia Akson amepokea msaada wa
vifaa mbalimbali kutokea kwa
Taasis ya Human Relief kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi wenye uhitaji maalum
wa ya Katumba ya mkoani Mbeya.
Akizungumza baada ya kupokea msaada huo
Tulia alisema, aliitembelea shule hiyo mapema mwezi huu na kusikia changamoto
zao mbalimbali.
Alisema, shule hiyo ina watoto wenye
ulemavu wa Ngozi na ulemavu wa viungo huku wote hao wakikabiliwa na changamoto
kadhaa za vifaa vitakavyowawezesha kusoma.
Alisema”msaada huu ni muhimu kwa wanafunzi
kwa kuwa utawawezesha kujisomea kwa Amani na furaha zaidi, wamekuwa kwenye
mazingira magumu ya kujisomea na nilichukua uamuzi wa kuwatafuta hawa wafadhiri
ambao nao wameitikia kwa wakati”.
Mkurugenzi wa Human Relief Foundation Sheikh Khalid Butchery (katikati) akizungumza.
Mkurugenzi wa Taasisi hiyo
ya Human Relief, Sheikh Khalid Butchery alisema Taasisi yake imeguswa na
harakati za Tulia katika kuisaidia jamii na imeguswa zaidi na changamoto
zinazoikabili shule hiyo na ndio maana imeamua kuisaidia.
Alisema Taasisi yake imetoa baiskeli 15
kwa ajili ya wanafunzi wenye ulemavu, mafuta maalum ya kupaka kwa wanafunzi
wenye ulamavu wa Ngozi katoni mbili, kofia 40 kwa ajili ya watoto hao, pia
karatasi maalum za kuandikia kwa watoto wenye ulemavu wa macho.
Pia Taasis hiyo imetoa mifuko 250 ya
saruji kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ya kujisomea hasa kwa kujenga darasa
jingine la watoto hao shuleni hapo.
Naye mmiliki wa kampuni ya mafuta ya
Bigbon Mohamed Bahashwan na mwenzake Shafiq Dhalla anaemiliki kampuni ya
Quintex walitangaza kuongeza mifuko mingine 250 ya saruji ambayo Tulia alisema
itapelekwa sekondari ya Iyela.
Tulia alisema, ataendelea kusaidia jamii
zenye uhitaji kwa kuwa kama mzazi anaguswa na maendeleo ya elimu na hasa kwa
watoto wenye uhitaji maalum.
Naibu Spika wa Bunge la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Ackson akipokea Msaada wa kofia kwa
ajili ya Watoto wenye ulemavu wa ngozi wanaosoma katika shule ya Walemavu
Katumba kutoka kwa Mkurugenzi
wa Human Relief Foundation Sheikh Khalid Butchery (kulia), mmiliki wa kampuni ya mafuta ya Bigbon Mohamed Bahashwan.
Naibu Spika wa Bunge la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Ackson,akipokea alama ya Tasisi ya
Human Relief Foundation kutoka kwa Mkurugenzi wa Human Relief
Foundation Sheikh Khalid Butchery.
Moja ya vifaa vilivyotolewa.
Naibu
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Ackson akizungumza
na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam Januari 26, 2018 mara baada ya kupokea
Msaada wa Vifaa kwa ajili ya shule ya Walemavu ya Katumba iliyopo Mkoani Mbeya
Wilaya ya Rungwe (kulia) Mkurugenzi wa Human Relief Foundation Sheikh
Khalid Butchery.
Naibu Spika wa Bunge la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Ackson,akiwa katika picha ya pamoja
na wajumbe wa Tasisi ya Human Relief Tanzania
Waandishi wa habari wakiwa kazini.
(Picha zote na Philemon Solomon-Mtazamonews.com)
0 Comments