Random Posts

Kamati za Kudumu za Bunge Zafanya Uchaguzi wa Wenyeviti na Makamu Wenyeviti.

Mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi na Madawa ya kulevya, Mhe. Matter Salum akiongoza uchaguzi wa kumchagua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo katika kikao kilichofanyika jana katika kumbi za Bunge Mjini Dodoma.
Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge wakifuatilia uchaguzi wa kumteua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo uliofanyika jana katika kumbi za Bunge Mjini Dodoma.
 Mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Mhe. Eng. Ramo Makani akiongoza uchaguzi wa kumchagua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo katika kikao kilichofanyika jana katika kumbi za Bunge Mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, Mhe. Jasson Rweikiza (katikati) akizungumza na Wajumbe wa kamati hiyo baada ya kuteuliwa kuendelea tena na nafasi hiyo katika uchaguzi uliofanyika jana katika kumbi za Bunge Mjini Dodoma. Wa nne kulia waliokaa, ni Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Mwanne Mchemba


(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

Post a Comment

0 Comments