Random Posts

Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya Ilala Kimewapa pole Wananchi wote Waliopata Athari za Maafa Kutokana na Mvua

Chama cha mapinduzi CCM  wilaya ilala kimewapa Pole wananchi wote waliopata athari za maafa kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha, jijini Dar es salaam.

Taarifa hiyo imetolewa na  katibu mwenezi wa chama hicho wilaya ya Ilala Said sidde na ambapo ametoa wito kwa viongozi wa chama ngazi zote kutoa ushirikiano wa kutosha kwa waathirika, ikiwa ni pamoja na kutembelea maeneo yao na kutoa msaada wa Hali na Mali.

Aidha ameongeza kuwa misaada hiyo ni pamoja na njia za kuwahifadhi waathirika hususan wanawake, watoto, wazee pamoja na wasiojiweza kwa kushirikiana na viongozi wa serekali za mtaa.

 "tutumie nafasi yetu kwa kushirikiana na viongozi wa serikali za mitaa na serikali kuu kufahamu kiwango cha uharibifu wa Mali na miundombinu pamoja na takwimu za walioathirika"alisema sidde.

Hata hivyo amewataka watu wote kushirikiana kumuombe mwenyezi mungu kwa imani zao ili  kupate mvua za wastani zisizo na madhara kwa binadamu, mifugo na Mali.

Post a Comment

0 Comments