Random Posts

RC Tabora: Aagiza Ukaguzi wa Ujenzi vya Vyumba Vitatu vya Madarasa Katika Shule ya Msingi Ilolangulu

NA TIGANYA VINCENT
RS TABORA
5 May 2018
SERIKALI Mkoani Tabora imeagiza kusimamishwa mara moja ujenzi wa vyumba vitatu vya madarsa katika  Shule ya Msingi Ilolangulu Wilayani Uyui hadi hapo ukaguzi maalumu wa fedha zilizotumika kujenga zinalingana na zinalingana na michango iliyotolewa na wananchi ya milioni 11.
Agizo hilo limetolewa jana Wilayani Uyui na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati wa ziara yake katika maeneo mbalimbali kwenye kampeni kupambana na utoro na kukagua miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa unafanywa na wananchi kwa kushirikiana na wadau wengine.
Alisema kuwa ameamua kuzuia kwa muada wa siku ujenzi wa madarsa hayo matatu hadi hapo atakapopata ufafunuzi wa kuridhisha juu ya matumizi ya shilingi milioni 11 zilizochangwa na wananchi zilivyotumika hadi kufikia madarasa hayo yalipofikia.
Mwanri aliongeza hatua hiyo itasaidia kuhakikisha kiasi cha milioni 25 zilizotolewa na Equip T kupitia Serikali kuunga mkono juhudi za wananchi zinatumika sahihi kukamilisha sehemu iliyobaki na madarasa yatakayojengwa yawe yanalingana na thamani fedha iliyotolewa.
Alisema baada ya kukagua baadhi ya vifaa vilivyonunuliwa kwa ajili ya ukamilishaji wa madarasa hayo vinaonekana chini ya kiwango jambo linaloweza kusababisha kujengwa kwa madarasa ambayo hayana viwango vizuri na kufanya fedha ionekana kutolewa nyingi lakini halingani na thamani ya majengo.
Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa wa Tabora amemwagiza Mkurugenzi wa Mteandaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega na maeneo mengine kuhakikisha miradi inayojengwa kwa ajili ya wananchi ikiwemo ile ya elimu inazingatia matakwa ya kitaalamu na izingatie athari za kimazingira ili kuepuka usababishaji wa hasara kwa wananchi.
Mkuu wa Mkoa huo wa Tabora alilazimika kutoa tahadhari hiyo baada ya kutembelea boma la Shule shikizi ya Mwaguguli katika Halmashauri hiyo linalojengwa kwa nguvu za wananchi lakini limeanza kuonyesha nyufa hata kabla haijakamilika.
Alisema kabla ya kuanza kwa ujenzi wa boma lingine lenye vyumba viwili vya madarasa , ofisi moja ya walimu na matundu wanne ya vyoo kwa gharama ya milioni 62 zilizotolewa wa Equip –T kwa  lengo kuunga mkono juhudi za wakazi ni vema wakatuma mhandisi wa ujenzi, mkaguzi wa ndani , mtaalamu wa mazingira na wataalamu wengine kuchunguza sababu zilizo za nyufa katika bomu la  kwanza la shule tarajiwa hiyo.
Mwanri alisema hatua hiyo inalenga kujua kama mipasuko hiyo inasababishwa na udongo wa eneo husika au kuna mchezo ulifanywa na Mkandarasi ili hatua ziweze kuchukuliwa kwa ajili ya kuepusha hasara kwa wananchi na kujiridhisha kama eneo hilo sio sehemu ya Hifadhi ya Mistu.
Kwa upande wa Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Elimu Mkoa wa Tabora Suzzan Nussu aliwataka Wakurugenzi Watendaji na Wasimamizi wa Miradi yote ya ujenzi wa madarasa kuzingatia mafunzo na maelekezo waliyopatiwa ili kuepuka kuwa na majengo yaliyojengwa chini ya kiwango na kujikuta katika matatizo ya matumizi mabaya ya fedha za umma.
Alisema kwa wale wanaotekeleza Mpango wa Equip T ni vema wakazingatia maelekezo waliyopatiwa kuhusu ujenzi wa madarasa na Ofisi.

Nussu aliongeza kuwa ni vema maeneo yote ambayo wamepatiwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa wakajitahidi kufanya haraka kukamilisha ili watoto waache kutembea umbali mrefu kwenda shule

Post a Comment

0 Comments