NA TIGANYA VINCENT
RS TABORA
5 May 2018
MKUU wa Mkoa wa
Tabora Aggrey Mwanri amewahimiza wakazi Jisesa katika Kata ya Bukuko wilayani
Igunga kuhakikisha wanaendelea kujitolea
na kshiriki katika miradi ya ujenzi wa madarasa ili waweze kukamisha madarasa
yaliyobaki kwa ajili ya kuweka mazingira mazuri ya watoto wao kujisomea.
Alitoa wito huo
jana wilayani Igunga wakati akizungumza na wananchi wa Jisesa akiwa katika ziara
ya kuhimiza mapambano dhidi ya utoro na ujenzi wa majengo ya shule yaliyo bora.
Katika kutatua tatizo la ukosefu wa madarasa na kuunga mkono juhudi hizo
za wakazi wa Jisesa na Mbunge wa Jimbo la Igunga Dkt. Dalali Kafumu za ujenzi
wa madarasa , Mkuu wa Mkoa wa Tabora alitoa shilingi milioni moja, Mkuu wa
Wilaya ya Igunga John Mwaipopo alitoa laki tano na Halmashauri ya Igunga ilitoa
milioni tano.
Hatua hiyo inalenga kuongeza nguvu ili hatimaye maboma mawili ya
madarasa yalikwisha jengwa yakamilike na hatimaye na wanafunzi wawe mazingira
mazuri ya kujifunza kwa ajili ya kuongeza ufaulu wao.
Shule hiyo ya Jisesa ina wanafunzi 223 ambapo zaidi ya 80 hawa madarasa
ya kusomea na kulazimika kuchangia madarasa.
Hali hiyo imesababisha wanafunzi wa Darasa la VII na VI kusoma pamoja ,
Darasa la II, I na Chekechea nao kusoma pamoja na waliobaki kuwa hawana mahali
darasa la kujisomea.
Afisa Elimu Mkoa wa Tabora Suzan Nussu alisema licha ya watoto wa shule hiyo
kukosa madarasa ya kujifunzia wamekuwa miongoni shule inayofanya vizuri katika
ufaulu wa mtihani wa kuhitimu darasa la saba na stadi kusoma , kuandika na
kusabu(KKK).
Alisema kuwa licha ya shule hiyo inakabiliwa
na uhaba wa vyumba vya madarasa imekuwa ikifanya vizuri katika mitihani yake
ambapo katika mtihani wa kumaliza la saba 2017 Wilayani Igunga ilikuwa ya
kwanza kwa watoto ambao darasa lina idadi ya chini ya 40.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora ameanza
ziara ya kutembelea Halmashauri zote kuhimiza vita dhidi ya utoro, mimba za
utotoni na kuhimiza uibuaji wa miradi ya kilimo mashule kwa ajili ya kupata
chakula cha wanafunzi

0 Comments