Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora Kapteni (mstaafu) Mhe. George Mkuchika (Mb) akisisitiza jambo kwa
Balozi wa Uswiss nchini Tanzania na Zambia, Mhe. Florence Tinguely Mattli (hayupo
pichani) wakati wa kikao na Balozi huyo ofisini kwake leo jijini Dodoma.
Balozi wa Uswiss nchini Tanzania na Zambia, Mhe. Florence Tinguely
Mattli akizungumza na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora, Kapteni (mstaafu) Mhe. George Mkuchika (Mb) hayupo
pichani wakati wa kikao leo jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala Bora Kapteni (mstaafu) Mhe. George Mkuchika (Mb) akipokea zawadi toka kwa Balozi wa Uswiss nchini
Tanzania na Zambia, Mhe. Florence Tinguely Mattli
aliyefika ofisini kwake jijini Dodoma kujitambulisha.
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
Kapteni (Mstaafu) Mhe. George Mkuchika (Mb) ameishukuru Serikali ya Uswiss kwa
ushirikiano wake katika sekta mbalimbali ikiwamo masuala ya utawala bora.
Mhe.
Mkuchika amesema hayo leo katika kikao na Balozi wa Uswiss nchini Tanzania na
Zambia, Mhe. Florence Tinguely
Mattli kilichofanyika ofisini kwake jijini Dodoma.
Mhe. Mkuchika amesema, Serikali ya Uswiss
imekuwa ikitoa ushirikiano mkubwa kwa Tanzania katika masuala ya utawala bora
ambayo wafadhili wengi hawayapi kipaumbele.
Amezitaja nchi nyingine zinazoshirikiana na
Serikali ya Tanzania katika masuala ya utawala bora kuwa ni Uingereza kupitia Shirika
lake la Maendeleo la DfID na Marekani kupitia Shirika lake la Misaada la USAID.
Aidha, Mhe. Mkuchika amesema, Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Uongozi wa Rais wake, Mhe. Dkt. John
Pombe Magufuli inahakikisha suala la utawala bora linazingatiwa katika
utekelezaji wa majukumu mbalimbali.
Kwa upande wake, Balozi wa Uswiss nchini
Tanzania na Zambia, Mhe. Florence
Tinguely Mattli ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa
jitihada wanazozifanya katika utekelezaji wa masuala ya utawala bora na ameahidi
kuendeleza ushirikiano.
0 Comments