Watoto tisa wenye matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo
wanaondoka leo tarehe 28/5/2018 kwenda nchini Israel kwa ajili ya matibabu ya
moyo. Katika safari yao ya matibabu nchini humo watoto wataambata na
wauguzi pamoja na wazazi wao.
Safari hiyo ya matibabu nchini Israel inahusisha watoto
wenye umri wa miezi tisa hadi miaka 14 imeratibiwa na Taasisi ya Moyo
Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto
(Save a Child’s Heart – SACH) ya nchini humo.
Taasisi yetu inatibu magonjwa mengi ya moyo (kwa
asilimia 90) kwa watoto kupitia wataalamu wazalendo tulionao. Hata
hivyo tunamkataba na Israel kwa baadhi ya wagonjwa wachache ambao ni asilimia
10 wanaohitaji utaalamu wa hali ya juu zaidi kuliko uliopo hapa nchini kwa sasa.
Tunaushirikiano mzuri na nchi ya Israel kwani gharama za
matibabu ya watoto hawa zinagharamiwa na SACH. Aidha tuna madaktari bingwa wa
magonjwa ya moyo sita na wauguzi wanne ambao wamesoma nchini Israel
na hivi sasa wanatibu wagonjwa katika Taasisi yetu. Daktari wetu mmoja na
wauguzi wawili bado wanaendelea na masomo nchini humo hii itasaidia kwa siku za
mbeleni zaidi ya asalimia 95 ya watoto watatibiwa hapa nchini.
Hili ni kundi la sita la watoto kwenda kutibiwa
magonjwa ya moyo nchini Israel tangu mwaka 2015 ambapo Taasisi ya Moyo ilianza
ushirikiano na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart –SACH)
wa kuwapeleka wagonjwa nchini humo. Hadi sasa watoto 56 wameshatibiwa
nchini humo na wanaendelea vizuri.
Taasisi inaendelea kutoa wito kwa wazazi na walezi wasisahau
kupima afya za watoto wao pale watakapoona kuna hali ya tofauti katika ukuaji
wa mtoto kwani magonjwa mengi ya moyo yanaanzia utotoni. Mtoto akianza kuuguwa
magonjwa ya moyo wazazi wengi wanadhani ni matatizo ya kifua baada ya kumfikisha
mtoto Hospitali na kufanyiwa vipimo ndipo inagundulikwa kuwa mtoto
anasumbuliwa na magonjwa ya moyo.
Kwa wamama wajawazito wafanye uchunguzi (Fetal
Echocardiography) wa kuangalia kama mtoto aliyeko tumboni anamatatizo ya moyo
au la. Kupitia kipimo hiki mtoto akigundulika kuwa na tatizo la
moyo ataweza kupatiwa matibabu kwa wakati na hivyo kuwa na afya
njema kama watoto wengine.
Imetolewa
na :
Imetolewa
na:
Kitengo
cha Uhusiano
Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete
28/05/2018


0 Comments