Wednesday 29 November 2023

TEWW yazindua programu ya IPOSA katika mikoa sita

Katibu Tawala Mkoa Singida, Dkt. Fatma Mganga, akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mpango wa Elimu Changamani kwa Vijana walio nje ya Mfumo Rasmi (IPOSA) kupitia ufadhili wa Serikali ya Korea chini ya shirika la  Koica uliofanyika Novemba 28, 2023 mkoani  hapa. 

.....................................

Na Dotto Mwaibale, Singida

TAASISI  ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) imezindua  awamu ya pili ya Mpango wa Elimu Changamani kwa vijana walio nje ya shule (MECHAV/IPOSA) kwa ufadhili wa Sh. Milioni 6 dola za Kimarekani zilizotolewa na  Serikali ya Korea Kusini  kupitia Shirika la Koica ambao umezinduliwa Novemba 18, 2023 mkoani Singida  ukilenga kuwakwamuwa vijana kielimu na kiuchumi.

Katibu Tawala Mkoa Singida, Dkt. Fatma Mganga akizindua mpango huo mkoani hapa kwa niaba ya mikoa sita ambayo mpango huo utatekelezwa kwa awamu ya pili  ametoa ushauri kwa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia kuangalia upya sera na sheria inayoelekeza mwanafunzi asiye hudhuria shuleni kwa muda wa siku 90 kufutwa baada ya kupoteza sifa za kuwa mwanafunzi.

Dkt. Mganga ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo  alisema  sheria hiyo imekuwa ikiongeza idadi kubwa ya vijana walio nje ya Mfumo Rasmi wa Elimu  Changamani (IPOSA).

Alisema kuwepo kwa sheria hiyo kunaweza kuwafanya baadhi ya wazazi na walezi wasiopenda watoto wao kusoma kuwazuia wasiiende shuleni kwa muda huo kwa kuwa watakuwa wamejiondoa wenyewe hivyo kusababisha idadi kubwa ya watoto kuwepo mitaani bila ya kujua kusoma, kuandika na kuhesbabu.

Dkt. Mganga aliwataka maafisa elimu, watendaji wa Kata, maafisa Tarafa na viongozi wengine kufanya jitihada za makusudi katika maeneo yao ili kuwabaini watoto ambao hawaendi shuleni ili wajue kwanini wapo nyumbani na kuwarudisha shuleni.

Alisema Mkoa wa Singida wanafunzi wanaomaliza darasa la saba ufaulu wao haupo vizuri upo asilimia 76 jambo ambalo  si zuri ukilinganisha na mikoa mingine.

Alisema mpango huo wa IPOSA ni fursa kwa vijana walio nje ya shule kwa kuwa unalenga kupunguza idadi ya vijana walioko mitaani kwa kuwajengea stadi za maisha, stadi za ujasiriamali, stadi za Kusoma, Kuhesabu na Kuandika na stadi za Ufundi wa Awali na hatimaye kupata fursa za kujiajiri au kuajiriwa.

"Mpango huu umezingatia dhima ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ya kutoa Elimu bora kwa wote, Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014, toleo la 2023 inayolenga pia kutoa mafunzo ya amali kwa vijana na Mpango wa Maendeleo ya Elimu," alisema Dkt.Mganga.

Alisema mpango huo unaendeleza utekelezaji wa azma ya Serikali kutoa Elimu kwa Watoto na Vijana kupitia mfumo rasmi na usio rasmi.

Aidha,  Dkt. Mganga alisema amefarijika kufahamu kuwa baada ya utekelezaji wa wa mpango huo katika mikoa 10  sasa wanaelekea kwenye upanuzi wa huo kwenye mikoa sita zaidi na kufikia mikoa 16 ya Tanzania bara na kuitaja mikoa hiyo sita kuwa ni Pwani,Tanga, Manyara, Simiyu, Singida na Shinyanga kwa ufadhili wa KOICA.

Alisema mikoa hiyo ilipatikana kwa kuzingatia uwepo wa vijana wengi kati ya umri wa miaka 14 na zaidi waliopo nje ya shule, utayari wa mikoa katika utekelezaji wa mpango huo , uwepo wa walimu wa ufundi na uwepo wa miundombinu pamoja na PPTCs.

Alisema mpango huo ulioanza kutekelezwa kwa ufadhili wa KOICA zitajengwa karakana mpya 30 kwa ajili ya mafunzo, ununuzi wa  vifaavipya vya kufundishia ufundi na kufadhili mafunzo ya muda mfupi ya walimu 240 na mafunzo ya diploma ya elimu ya watu wazima na teknolojia kwa walimu 120.

Aliongeza kuwa vilevile vitajengwa vituo 3 vikubwa vya mafunzo ya walimu watakaosoma diploma ya elimu ya watu wazima na teknolojia katika mikoa ya Tanga, Manyara na Shinyanga.

Alisema kwa hatua hiyo inadhihirisha jitihada walizozionesha na kuwapa imani wafadhili na kuendelea na awamu ya pili, ambapo pamoja na mambo mengine walifanikiwa kudahili vijana 12,000 (Me 5,406, Ke 6,594) kwa programu ya muda mrefu na 30,183 kwa programu ya muda mfupi katika kipindi cha miaka mitatu kwa Mikoa kumi ya Kigoma, Tabora, Mbeya, Songwe, Iringa, Njombe, Dodoma na Dar es salaam kwa ufadhili ya UNICEF na Mkoa wa Shinyanga kwa ufadhili wa Care International na Mkoa wa Rukwa kwa ufadhili wa Plan Internatioanal na   kuwa kwa awamu hii ya pili wamelenga kudahili vijana 52,000 mpaka ifikapo mwaka 2026.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Kamishna wa Elimu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Oscar Msalila alisema Mpango wa IPOSA ni matokeo ya juhudi za pamoja kati ya wizara hiyo, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Taasisi ya Elimu ya Watu wazima na wadau wa maendeleo UNICEF.

Alisema kupitia mpango wa IPOSA vijana wenye umri kuanzia miaka 14 wameweza kujengewa stadi za ujasiriamali na stadi za ufundi wa awali ili waweze kujikomboa kiuchumi na kuchangia uchumi wa Taifa.

Alisema katika utekelezaji wa mpango huo wa  IPOSA  chini ya UNICEF, Care International na Plan International vijana waliofuzu mafunzo yao wameweza kuunda vikundi vya kijasiriamali ambavyo vimewawezesha kufanya biashara na kujipatia kipato.

Msalila alivitambulisha vikundi vichache vya IPOSA kutoka Mbeya na Kigoma ambayo vimeweza kuanzisha bidhaa za taulo za kike ambazo zinaweza kutumika zaidi ya mara moja pamoja na bidhaa za samani mbalimbali.

Alisema ubunifu wa bidhaa hizo ni muhimu kwa Taifa la Tanzania hasa kwa watu wa kipato cha chini, madhalani wale ambao si rahisi kumudu gharama za kununua taulo za kike zilizozoeleka ambazo bei zake kwa kiasi fulani ni kubwa kidogo.

Alisema zaidi ya kiwanda hicho cha taulo za kike  mpango huo umeweza kuzalisha vijana wabobezi katika fani ya umeme na wameweza kutengeneza mifumo ya kibunifu ambayo ni suluhisho wa ulinzi nyumbani.

Mkurugenzi Mkazi kutoka Taasisi ya Koica, Manshik Shin, alisema Koica ni chombo muhimu kwa Serikali ya Korea ambacho kinafanya kazi katika miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye nchi 46 duniani ikiwepo Tanzania na kuwa hapa nchini ilianzishwa rasmi mwaka 1991.

Alisema Koica ilifungua ofisi yake katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2002 na kuwa katika nchi za Afrika Tanzania ni nchi ya pili kunufaika na miradi inayofadhiliwa na shirika hilo ambapo mpaka sasa jumla ya Sh.Bililioni 22 zimekuwa zikitolewa kufadhili miradi mbalimbali kila mwaka.

Shin alisema Koica imekuwa ikiisadia Tanzania Bara na Visiwani kwenye eneo la Elimu, Afya, Maendeleo ya Vijijini, Eneo la Jinsia, TEHAMA na masuala mbalimbali ya mtambuka.

Alisema katika sekta ya elimu Koica imekuwa ikifadhili shughuli za programu za ufundi, sayansi, uhandisi na hesabu ili kukuza uwezo wa vijana na waweze kujiajiri.

Afisa Elimu Mkoa wa Singida, Dkt.Elpidius Baganda alisema mpango huo kwa Mkoa wa Singida umefika wakati muafaka kwani kuna vijana wenye umri kati ya miaka 14 hadi 19 zaidi ya 15,000 wenye sifa za kujiunga kwenye mpango huo, kunavija ambao hawakubahatika kwenda shule 672 na walioacha shule 1064, wanafunzi waliomaliza darasa la saba lakini hawakupa fursa ya kuendelea na masomo ni 12, 013, waliomaliza kwa kupitia MEMKWA ni 1260 na walioacha shule kwa changamoto mbalimbali zikiwepo mimba ni 398.Katibu Tawala Mkoa Singida, Dkt. Fatma Mganga, ambaye alikuwa mgeni rasmi akihutubia kwenye uzinduzi wa mpango huo.Mkurugenzi Mkazi kutoka Taasisi ya Koica, Manshik Shin, akizungumzia jinsi shirika hilo linavyofadhili miradi mbalimbali hapa nchini.Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima,   Profesa Michael Ng;umbi, akizungumza kwenye uzinduzi huo.Kwa upande wake Mwakilishi wa Kamishna wa Elimu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Oscar Msalila akizungumza kuhusu mradi huo.Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima, Profesa Sotco Komba, akizungumzia taasisi hiyo jinsi inavyoshiriki katika mpango huo.Mkurugenzi Idara ta Elimu Mbadala na Watu Wazima Zanzibar, Mashavu Ahamad Faga, akizungumza kwenye uzinduzi huo.Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Ernest Hinju akizungumza kwenye uzinduzi huo.Afisa Elimu Watu Wazima na Elimu nje ya Mfumo Rasmi Wilaya ya Kasulu Mkoa wa Kigoma,  Felician Ferdnand (kushoto) akiwa na  Mratibu wa Kituo cha Ufundi (TRC) cha Mbalizi Mkoa wa Mbeya Mhandisi Lwitiko Mwakatumbula ambapo walipata fursa ya kuelezea mafanikio ya mpango huo wa IPOSA katika mikoa yao kwenye uzinduzi huo..

Afisa Elimu Mkoa wa Singida, Dkt.Elpidius Baganda, akizungumza kwenye uzinduzi huo.
Viongozi wa dini wakiwa kwenye uzinduzi huo. Katikati ni Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nasoro.
Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Singida wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Wanufaika wa programu hiyo wapo kwenye uzinduzi huo.

Uzinduzi ukiendelea.
Uzinduzi ukiendelea.
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Uzinduzi ukiendelea.
Wimbo wa Taifa ukiimbwa.
Viongozi meza kuu wakishiriki kuimba wimbo wa Taifa.
Wimbo wa Taifa ukiimbwa.
Mshauri wa Jeshi la Akiba Mkoa wa Singida Kanali Rhinoceros Magemeson,(kushoto)_ na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna Msaidi wa Polisi (ACP) Stella Mutabihirwa wakipiga saluti wakati wimbo wa Taifa ukiimbwa.

Wasanii wa Kikundi cha Mbaramwezi wakitoa burudani wakati wa uzinduzi huo.
Afisa Habari Manispaa ya Petronella Msechu (kushoto) na  Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Manispaa ya SingidaUpendo Naftali,wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Afisa Elimu Watu Wazima na Elimu nje ya Mfumo Rasmi Wilaya ya Kasulu Mkoa wa Kigoma, Felician Ferdnand , akizungumzia mafanikio ya mpango huo mkoani humo.
Mratibu wa Kituo cha Ufundi (TRC) cha Mbalizi Mkoa wa Mbeya Mhandisi Lwitiko Mwakatumbula akielzea jinsi mpango huo ulivyowainua kiuchumi vijana mkoani humo.
Taswira ya uzinduzi huo.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida , Yagi Kiaratu, akizungumza kwenye uzinduzi huo.
Katibu Tawala Mkoa Singida, Dkt. Fatma Mganga, akimkabidhi cheti Mwakilishi wa  Shirika la UNICEF, Pantalee Kapichi kwa kutambua kazi kubwa inayofanywa na shirika hilo kwa kusaidia katika maeneo mbalimbali.
Afisa Miradi ya Elimu Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Selanda Zahoro Jamadari  akionesha cheti cha kutambua mchango wa TEA katika sekta ya elimu hapa nchini. 
Viongozi wa meza kuu wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Picha ya pamoja na waratibu wa uzinduzi huo.
Picha ya pamoja na wadau wa maendeleo.
Picha ya pamoja na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama Mkoa wa Singida.

No comments:

Post a Comment