Subscribe Us

header ads

RAIS DKT. SAMIA AZINDUA RASMI HUDUMA ZA USAFIRI WA TRENI YA KISASA (SGR)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuzindua jengo la Stesheni ya Treni ya Kisasa (SGR) katika eneo la Kilometa 0 Jijini Dar es Salaam Agosti 01, 2024.
Taswira ya jengo la Stesheni ya Treni ya Kisasa (SGR) katika eneo la Kilometa 0 Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuzindua jengo la Stesheni ya Treni ya Kisasa (SGR)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akitembelea jengo la Stesheni ya Treni ya Kisasa (SGR).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania Masanja Kadogosa mara baada ya kuwasili Stesheni ya Treni ya Kisasa (SGR) Jijini Dar es Salaam tarehe 01 Agosti, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Taarifa kuhusu Chumba Maalum cha kuongozea Treni ya Kisasa (SGR) katika eneo la Stesheni Kilometa 0 Dar es Salaam tarehe 01 Agosti, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuzindua safari za Treni ya Kisasa  (SGR) kuanzia eneo la Stesheni Kilometa 0 Jijini Dar es Salaam hadi Dodoma tarehe 01 Agosti, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na abiria mbalimbali waliokuwa wakisafiri na Treni ya Kisasa ya Umeme (SGR) kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma mara baada ya uzinduzi katika eneo la Kilometa 0 Stesheni Jijini Dar es Salaam tarehe 01 Agosti, 2024.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Pugu Jijini Dare es Salaam wakati akielekea Dodoma kwa Usafiri wa Treni ya Kisasa ya (SGR). Mhe. Rais Dkt. Samia amezindua Rasmi huduma za Usafiri wa Treni ya Kisasa (SGR) kuanzia eneo la Kilometa 0 Stesheni Jijini Dar es Salaam- Morogoro hadi Dodoma tarehe 01 Agosti, 2024.

Post a Comment

0 Comments