Random Posts

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara Linawashikilia Watuhumiwa 46 kwa Matukio Matatu Tofauti

Kamanda wa Polisi mkoani mtwara Lucas Mkondya hivi karibuni akionyesha baadhi ya namba za pikipiki zilizokamatwa kwenye msako uliofanywa na jeshi hilo na kufanikiwa kukamata pikipiki kumi katika Kijiji cha Chikongo wilaya ya Tandahimba mkaoni hapa.
Kamanda wa Polisi mkoani mtwara Lucas Mkondya hivi karibuni akionyesha baadhi ya vioo vya pikipiki zilizokamatwa kwenye msako uliofanywa na jeshi hilo na kufanikiwa kukamata pikipiki kumi katika Kijiji cha Chikongo wilaya ya Tandahimba mkaoni hapa.
Kamanda wa Polisi mkoani mtwara Lucas Mkondya hivi karibuni akionyesha baadhi ya pikipiki zilizokamatwa kwenye msako uliofanywa na jeshi hilo na kufanikiwa kukamata pikipiki kumi katika Kijiji cha Chikongo wilaya ya Tandahimba mkaoni hapa.

Na.Martina Ngulumbi


JESHI la Polisi Mkoa wa Mtwara linawashikilia watuhumiwa 46 katika matukio matatu tofauti ikiwemo wahamiaji haramu 23, wizi wa pikipiki 13 na uchochezi kwa njia ya mitandao 13.

Akizungumzia matukio hayo hivi karibuni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara Lucas Mkondya amesema kuwa jeshi hilo linawashikilia wahamiaji 23 kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha sheria.

Amesema kuwa watuhumiwa hao walikutwa katika eneo la Chikongola Wilaya ya Mtwara baada ya askari wa doria kupewa taarifa na raia wema wanaoishi karibu na nyumba za wageni waliyofikia wageni hao zao kihinga na lantumento.

Mkondya amesema kuwa wingi wa watu hao uliwashtua watanzania wenye nia njema ambao walitoa taarifa kwa jeshi la polisi ambapo baada ya ubekuzi ilibainika kuwa wapo watu 23 kutoka mataifa matatu tofauti ambapo raia wa kongo 13, Rwanda 7 ma 2 kutoka Burundi.

Ambapo katika mahojiano ya awali liliongesha kuwa wahamiaji hao walikuwa wakisafirishwa kwenda ufaransa kwa kupitia  visiwa vya Comoro.

Katika tukio lingine kamanda amesema kuwa wanawashikilia watu 13 ambao wanajihusisha na mtandao wa wizi wa pikipiki katika kijiji cha chikongo wilayani tandahimba.

Aidha jeshi hilo limebaini kuwa mtandao umegawanyika katika makundi matatu ambapo kundi la kwanza ni wezi wanaofanya wizi wa pikipiki maeneo mbalimbali kisha kuzipelekea kwa wanaohifadhi na mwisho kwa wauzaji ambapo kundi hilo linaongozwa na Mohamed Juma (simba).

Katika tukio lingine Jeshi la Polisi linawashikilia wanafunzi 9 wa Chuo Kikuu cha Stella Maris Mtwara na Daktari wa Hospitali ya Mission Nanyamba halmashauri ya mji Nanyamba.

Amesema kuwa watuhumiwa hao kwa nyakati tofauti wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii ikiwemo ‘Watsapp’ na Telegram’ kwa kumkashifu Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na kuhamasisha maandamano yasiyo na kibali ya April 26 mwaka huu.

Jeshi la polis linatoa onyo kali kwa watu kujiepusha kutumia mitandao ya kijamii vibaya  na kupelekea uvunjifu wa sheria za nchi ambapo katika matukio yote upelelezi bado haujakamilika.

Post a Comment

0 Comments