Shekhe Mkuu na Mufti wa Tanzania Aboubakar Bin Zuber Bin Ali
amepongeza ushirikiano uliopo baina ya baraza la waislamu la Mkoa pamoja na serikali ya Mkoa wa Rukwa katika
kutatua kurekebisha au kuyaweka sawa masuala mablimbali kwa maslahi ya
watanzania.
“siku zote huwa nawaamnbia viongozi wangu hawa wa baraza kwamba
wafanye kila wanachokifanya lakini wahakikishe kuwa wanajenga mahusiano mazuri
na serikali ya mahala walipo, baada ya kujenga mahusiano na wananchi wa dini
zote basin a serikali pia na katika eneeo hili ninapowauliza panaonesha pana
mashirikiano mazuri, cha kusema ni kwamba ushirkinao na uhusiano uendelee na udumu
vizuri kwasababu ndio utakaoweza kujenga nchi yetu katika masuala yote ya maendeleo,”
alisema.
Picha ya pamoja
Wakati akisoma taarifa ya Mkoa, mwakilishi wa mkuu wa Mkoa wa Rukwa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Khalfan Haule amepongeza juhudi mbalimbali zinazofanywa na waislamu katika kuiletea nchi maendeleo na kumuomba mufti wa Tanzania kuikumbuka Rukwa katika mipango yao mbalimbali ya uwekezaji katika sekta ya afya, maji, elimu na viwanda.
“Baada ya serikali kutangaza elimu bure kuna mafuriko ya wanafunzi huko mashuleni, hii inaonesha kwamba bado miundombinu ya elimu bado haitoshelezi hivyo tunahitaji kwenye eneo hilo ushirikinao wa kujenga shule za msingi, sekondari na hata vyuo, sisi ni eneo la pembezoni lakini tunapenda kuliita eneo la kipaumbele hivyo kwenye mipango yako basi utuweke kwenye eneo la kipaumbele,” Alisema.
Mufti wa Tanzania atafanya ziara ya siku mbili katika Wilaya ya Sumbawanga pamoja na Nkasi, akizindua na kuweka mawe ya msingi katika misikiti pamoja na kituo cha afya kilichopo kata ya kirando, Wilayani Nkasi.
Mufti Shekh Mkuu wa Tanzani Aboubakar Bin Zuber (katikati) pamoja na
mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Khalfan
Haule (kuliani kwake) na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Aboubakar
Kunenge (kushoto kwake) katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati ya
Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Rukwa.


0 Comments