Na Mwandishi Wetu
Katibu mkuu wa chama Cha ACT wazalendo Dorothy semu
amewataka wanachama wa chama hicho kuwa wazalendo na chachu ya kuchochea
maendeleo ya watanzania.
Hayo ameyasema jijini Dar es salaam wakati akipokea zaidi
ya wanachama wapya 100 waliojiunga na chama hicho ambapo amewasisitiza
kushirikiana pamoja na viongozi katika kujenga chama chenye ueledi na udhubutu
wa kuhoji kwani ndio viongozi wa kesho.
Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha Act mkoa wa Dar
es salaam Salumu Sudi amewataka wanachama hao kuanzisha matawi kwenye maeneo
yao na kugombea nafasi mbalimbali zilizowazi ndani ya chama hicho.
Hata hivyo ameongeza kuwa wanatarajia kuanzisha ligi ya
mpira wa miguu ya chama cha Act mwezi Mei mwaka huu ambayo itahusisha majimbo
yote ya mkoa wa Dar es salaam ikilenga kuibua vipaji vya vijana pamoja na
kukuza ushirikiano ndani ya jamii.



0 Comments