Ofisa
msaidizi wa misitu Bagamoyo,Jonathan Mpangala,akionyesha mipaka ambayo
imewekwa katika msitu wa hifadhi ya Taifa Uzigua ,wakati mkuu wa mkoa wa
Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo (wa katikati mwenye suti)alipotembelea
msitu huo .
(Picha na Mwamvua Mwinyi)
Na Mwamvua Mwinyi,Bagamoyo
MKUU
wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo ,amekemea wenye nia ya
kuvamia msitu wa hifadhi -Uzigua wilayani Bagamoyo na atakaethubutu
kufanya hivyo tena atakiona.
Aidha
,ameutaka wakala wa misitu kanda ya Mashariki na wilayani hapo
,kuendelea kukaza uzi katika kufanya doria mbalimbali ili kudhibiti
uvamizi uliokuwepo kipindi cha nyuma .
Akizungumza
wakati alipokwenda kutembelea msitu wa Uzigua ,kujiridhisha kama
umeanza kurejesha uoto wake wa asili ,Ndikilo aliwaasa wananchi wakiwemo
wafugaji kuheshimu mipaka iliyopo na kuulinda msitu huo.
Alieleza
kuwa ,mwaka mmoja uliopita serikali ilifanya operesheni kali ambapo
waliondoa kaya zaidi ya 500 na maboma ya mifugo ya ng'ombe.
Hata
hivyo Ndikilo alisema ,kwasasa kumewekwa vigingi vidogo na vikubwa kama
mipaka vinaoonyesha upande wa msitu na upande wa wananchi hivyo
wasiendelee kuingilia mapito ya njia zinazopita msituni humo na msitu
wenyewe.
"Kuna
watu walivamia na wengine kuanza kuishi, kuvuna mbao, kukata miti kwa
ajili ya mkaa, kuni ,kufuga ng'ombe, kilimo, uchimbaji wa madini,na
kusababisha athari kubwa kwa msitu "
"Msitu
huu ni eneo la maji yanayoingia mto Wami, tuliondoa watu wote ,na leo
nimepita nimejiridhisha ,nimeona wanyama wameanza kurejea, wanyama wana
njia zao hususan tembo ,tumeona wameanza kupita kwenye mapito yao
kuelekea Wamimbiki,Saadan,;"
"Miti
imeanza kuota ,hivyo uoto wa asili unajirudia kama zamani, hivyo jamii
ikiiona inafukuzwa katika misitu ijue misitu ina manufaa kwao " alisema
Ndikilo.
Mkuu
huyo wa mkoa alichukua fursa hiyo kuiomba jamii iheshimu na kuilinda
misitu ya Uzigua ,Kazimzumbwi -Kisarawe,Ruvu Kusini na Wamimbiki ambao
wanapakana na Morogoro.
Nae
mkuu wa wilaya ya Bagamoyo ,alhaj Majid Mwanga,alisema tatizo lililopo
ni muingiliano wa mifugo hali inayosababisha wakulima kujiona kama
wanabaguliwa .
Alielezea ,tayari wamekaa katika vikao vyao wameomba fedha kwa ajili ya kuondoa wafugaji watakaokaidi .
Alhaj
Mwanga alisema, iifikie hatua jamii ikawa na uelewa wa makusudio ya
serikali yao na kuachana na tabia ya kutaka kuhalalisha mambo
yasiyokuwepo.
Ofisa
msaidizi wa misitu Bagamoyo,Jonathan Mpangala,alisema msitu huo
ulitangazwa na serikali kwa tangazo namba 466 ,la mwaka 1958.
Alisema
kuna wilaya tatu zilizoingilia msitu huo ikiwemo vijiji nane vya wilaya
ya Bagamoyo,vijiji viwili wilaya ya Kilindi na Handeni ni kijiji kimoja
.
Mpangala
alisema wakala wa misitu ulipoanza mwaka 2014 ndipo msitu wa Uzigua
ulipimwa tena rasmi ,ukiwa na ukubwa wa hekta 24,436 ama kwa tafsiri ya
hekari 61,090 ambako katika kipindi hicho walitoa tangazo la kuwataka
wavamizi waondoke.
Kwa mujibu wa Caroline Marundo kutoka TFS Kanda ya Mashariki, alimhakikishia mkuu wa mkoa ,kuwa msitu upo shwari .
Alisema hali inaridhisha kwani hakuna usumbufu wa watu kufanya shughuli zozote za kijamii.


0 Comments