Random Posts

Katibu MKuu-Prof. Mkumbo, Wizara ya Maji na Umwagiliaji Kuhamia katika Jengo lake jijini Dodoma

 Taswira ya Jengo la Wizara ya Maji na Umwagiliaji jijini Dodoma kabla ya kazi ya kukamilisha ujenzi wa mwisho ili lianze kutumika.
    Katibu Mkuu, Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof. Kitila Mkumbo akiangalia baadhi ya vyumba vya jengo litakalokua makao makuu ya wizara yake jijini Dodoma.
      Katibu Mkuu, Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof. Kitila Mkumbo akikagua mazingira ya kazi jijini Dodoma pamoja na Mkurugenzi wa kampuni ya  ujenzi ya Na Nandhra Bw. Daman Singh Nandhra. 
   Katibu Mkuu, Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof. Kitila Mkumbo akikabidhi mkataba mapema leo jijini Dodoma kwa Mkurugenzi wa kampuni ya  ujenzi ya Na Nandhra Bw. Daman Singh Nandhra ili kuanza kazi itayofanyika kwa miezi 12 .

         Katibu Mkuu, Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof. Kitila Mkumbo akiongea na baadhi ya wafanyakazi walioshuhudia mkandarasi akikabidhiwa kazi ya kukamilisha jengo la wizara yao lililopo jijini Dodoma.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



Wizara ya Maji na Umwagiliaji inatarajia kuhamia katika jengo lake jipya jijini Dodoma  ndani ya miezi kumi na mbili (12) kuanzia sasa. Jengo hilo lipo mtaa wa Posta na litagharimu kiasi cha shilingi bilioni sita.

Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof. Kitila Mkumbo amesema hayo wakati akimkabidhi mkataba mkandarasi atakayefanya kazi ya umaliziaji wa jengo hilo, ambalo lipo katika hatua za mwisho.

Prof. Mkumbo amesema anaelewa wapo watumishi ambao wanafanya kazi katika majengo tofauti, ila jengo hilo litakapokamilishwa wote watakua katika eneo moja, hivyo wawe na subira na waendelee kufanya kazi kwa kasi zaidi.

Ameongeza kuwa mkandarasi, kampuni ya ujenzi ya Na NDHRA, anatakiwa kufanya kazi bora na katika kipindi kilichoainishwa katika mkataba bila kuchelewa.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano
Wizara ya Maji na Umwagiliaji
10.05.2018

Post a Comment

0 Comments